Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2014

Mkapa aongoza mazishi ya Meja Jenerali Lupogo

Picha
Rais mstaafu akiweka shada la mauwa kwenye kaburi la meja Gerali msitafu Herman Lupojo wakati wa Mazishi RAIS mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa jana aliwaongoza viongozi mbalimbali na mamia ya waombolezaji katika mazishi ya Meja Jenerali mstaafu Herman Lupogo kwenye makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange pamoja na Jenerali Mstaafu Robert Mboma. Akisoma risala mara baada ya mazishi, Mwakilishi wa JWTZ, Meja Jenerali Gaudence Milanzi, alisema marehemu alifariki dunia Oktoba 19 mwaka huu kwa ugonjwa katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo alikokuwa akipata matibabu. Alisema, marehemu alimaliza elimu ya Kidato cha sita katika shule ya Sekondari Pugu mwaka 1956, baadaye akapata Stashahada ya Ualimu na Shahada ya kwanza ya Sanaa katika Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda. “Marehemu alijiunga na Jeshi

Adaiwa kuiba kichanga ili kulinda ndoa

Picha
JESHI la polisi mkoani Rukwa linamshikilia Magreth Juma (34), mkazi wa mtaa wa Chanji Manispaa ya Sumbawanga kwa tuhuma za wizi wa mtoto mchanga wa siku mbili. Mtuhumiwa huyo, alikamatwa Oktoba 22 asubuhi nyumbani kwake maeneo ya Chanji akiwa na mtoto huyo wa kike, ikiwa ni muda mfupi tangu aibiwe kutoka kwa mama mzazi huko Bangwe umbali wa takribani kilomita 15. Inadaiwa kuwa, awali taarifa zilifikishwa kituo cha polisi Sumbawanga majira ya alfajiri na mama wa mtoto huyo, Magreth Benisia (28), kuwa mtoto wake mchanga amepotea katika mazingira ya kutatanisha akiwa nyumbani kwake, ndipo polisi walianza msako mkali kwa kushirikiana na raia wema na muda mfupi baadaye waliweza kumkamata mtuhumiwa huyo akiwa na mtoto nyumbani kwake. Baada ya kukamatwa, katika maelezo yake ilibainika kuwa mama wa mtoto aliyeibiwa na ndugu wa mtuhumiwa waliwahi kuishi nyumba moja ya kupanga, hivyo kusababisha mtuhumiwa kumfahamu vizuri mama huyo wa mtoto na hivyo kuwa rah

Nec yaanza kuboresha Daftari la Wapigakura

Picha
Makamu mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi NEC hamid Mahamudu akizungumza na Waandishi wa Habari kulia ni mkurugenzi wa uboreshaji wa Daftari la wapiga kura Julias Malapa  Kitendawili cha tarehe rasmi ya Watanzania kupiga Kura ya Maoni itakayopitisha au kukwamisha Katiba Inayopendekezwa, kitateguliwa kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(Nec) baada ya kukamilisha uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapigakura Aprili mwaka ujao. Nec imebainisha hayo jijini Dar es Salaam jana ikieleza kuwa  tayari Serikali imetoa Sh15 bilioni za uboreshaji huo na kwamba utakamilika Serikali itakamilisha kutoa Sh270 bilioni zinazohitajika kwa ajili ya uboreshaji wa daftari hilo. Hadi sasa, kuna mkanganyiko kuhusu tarehe hiyo baada ya Rais Jakaya Kikwete kutaja mwezi Aprili  mwakani kama wakati wa kupiga kura hiyo, akipingana na Machi 15 iliyotolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema.  Makamu mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Hamid Mahmoud Hamid, alisema jijini Dar es Salaam ja

Afia gesti akitolewa mimba

MWANAFUNZI  wa kidato  cha tatu katika shule ya Sekondari ya Tongoni nje kidogo ya jiji la  Tanga,  (jina tunalihifadhi) amekutwa amekufa ndani ya nyumba ya kulala wageni alikopelekwa kutolewa mimba bila mafanikio. Kwa mujibu wa habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe mwanafunzi huyo alikutwa amekufa juzi katika nyumba ya kulala wageni iliyopo barabara ya 21 jijini Tanga. Mmoja wa wahudumu wa nyumba hiyo ya kulala wageni ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe alisema kwamba mwanafunzi huyo aliingia saa 4.00 asubuhi siku ya tukio akiwa ameambatana na kijana mmoja wakakodi chumba. “Baadaye alikuja mwanaume mmoja wa makamo ambaye alituuliza kama wameingia mwanafunzi huyo na mwenzake, tulipomwonyesha chumba  walichoingia naye akakodi chumba cha jirani ndipo tukaona wote wakijifungia kwenye chumba kimoja,” alisema mhudumu. Mhudumu huyo alisema baada ya muda wa saa moja, mvulana na mzee huyo wakaaga kwamba wanatoka
Picha
Baadhi ya askali Polis na mgambo wanaofanya kazi maeneo ya mipakani wametakiwa kuwa waadilifu na kuacha kuwanyanyasa wageni ambao ni Laia wa Burundi wanaokuwa wakiingia nchini kaika maeneo ya mipakani kufanya shughuli mbambali za ki ujirani mwema ili kuifanya dhana hiyo kuwa tija. Wito huo umetolewa na Mkuu wa wilaya ya kibondo mkoani kigoma Venance Mwamoto, wakati wa uzinduzi wa Soko la ujirani mwema lililojengwa mpakani mwa Burundi na Tanzani katika kijiji cha Kibuye kata ya Kumsenga. Katika hotuba yake iliyotolewa   kwa niaba yake    na Katibu tawala wa wilaya hiyo Bw, ayubu Sebabile   amesema kuwa kumekuwepo na vitendo kwa baadhi ya Askali polisi na Mgambo   kuwa toza pesa laia wa Burundi ambao wamekuwa wakiingia   Tanzaana kwa ajili ya kufanya biashara na metembezi ya kawaida maeneo ya mipakani hali ambayo ni kinyume na utaratibu na kupiga marufuku hali hiyo isirudiwe tena. Insert I Ayubu Sebabili katibu tawala Que in……………… Wananchi wanaoishi maeneo ya mipa

IPTL yaitia Doa serikali

Picha
Waziri mkuu Mizengo Pinda WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema Serikali imetiwa doa na kashfa ya IPTL ambapo zaidi ya Sh bilioni 200 zinadaiwa kuchotwa kwenye akaunti maalumu ya ‘Tegeta Escrow’, iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Pinda ambaye yupo jijini London, Uingereza kuhudhuria mkutano wa viongozi wa Afrika na wawekezaji wa Ulaya, aliyasema hayo alipokuwa akizungumza kwenye kipindi cha Dira ya Dunia kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) . Alisema madai hayo yametia doa Serikali kwa kuwa tayari wahisani wameshakata misaada waliyoahidi kuitoa kwa ajili ya bajeti ya 2014/15. Pinda alisema Serikali inafanya uchunguzi kupitia Takukuru na Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG). “Madai haya yanatia doa kwa maana yamesemwa na vilevile wanaweza (wahisani) kukata kutoa misaada, ni mbaya sana. Kwa bahati mbaya sana wakuu wamechukua hatua (kukata misaada) kabla hata matokeo yenyewe hayajajulikana,” alisema. Pin

Serikali yafunga migodi ya machimbo ya Dhahabu

Picha
Issa Machibya mkuu wa mkoa wa kigoma alipokuwa akiongea na wananchi wa kijiji cha kinyinya wilayani kakonko alipotoa amri ya kufunga migodi ya dhaabu Wananchi wa kijiji cha kinyinya wakiwa mkutanoni Kamati ya ulinzi usalama kigoma wakiwa ktk mkutano wa hadhara katika kijiji cha kinyinya  kwa ajili ya kuona namna ya kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji Serikali yafunga migodi ya machimbo ya Dhah abu Serikali imeamulu kufungwa kwa migodi yote ya machimbo ya Dhaabu iliyoko katika kata ya Nyamtukuza   wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma Amri imetolewa   na mkuu wa mkoa huo Issa Machibya alipokuwa akiongea na wananchi wa Kijiji cha Kinyinya wilayani humo kwenye mkutano wa hadhara alipokwenda kujionea hali halisi ilivyo baada ya kutokea mapigano ya wakulima wakigombea ardhi hatua iliyopelekea jumla ya watu watatu kupoteza maisha katika maeneo ya mashambani Uamzi huo umekuja baada ya wakazi wa wakijiji hicho kutoa maelezo yao kuwa chanzo cha vulugu ni ni

Watu wawili wafa katika mapigano kugombania ardhi na ukabila

Picha
Wananchi wa kijiji cha Kinyinya wakimsikiliza Dc Askali Polis wilaya ya Kakonko waliokuwa wanalinda usalama wakati wa mapigano kati ya wakulima Waha na Wasukuma Kijiji cha kinyinya na Kakonko ambapo watu waili walipoteza maisha Venance Mwamoto kaimu mkuu wa wilaya ya kakonkoalopokuwaakizungumza na wakazi wa kijiji cha kinyinya Tarafa ya Nyaronga Kakonko wakati wa vurugu za kugombea ardhi kati ya wasukuma na waha Watu wawili wafa katika mapigano kugombania ardhi na ukabila Nyumba ya mkulima kijiji cha Kinyinya kakonko Watu wawili wamekufa na wengine hawajulikani walipo baada ya kuzuka mapigano kwa ajili ya kugombania ardhi kati ya kabila la Wasukuma na Waha   katika kijiji cha kinyinya   kata ya nyamtukuza wilaya ya Kakonko mkoa wa Kigoma   Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw Justini Kilegea, amesema kuwa   mapigano hayo yamewahusisha watu wa kabila la Wasukuma dhidi ya kabila la Waha   usiku wa kuamkia jana baada watu wa kabila la   wasukuma wanaoishi mash

Profesa Shivji: Migogoro ya ardhi ni adui wa maendeleo ya wananchi

Kwa muda mrefu, Serikali imekuwa ikianzisha mipango, sera, miradi na mikakati mbalimbali yenye lengo kuinua uchumi nchini. Licha ya mipango hiyo kuwapo, bado kumekuwa na ugumu katika kufikia mafanikio yaliyotarajiwa kutokana na sababu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuwa na mipango na mikakati mingi kwa wakati mmoja pamoja, hali kadhalika uwapo wa migogoro ya ardhi katika vijijini vingi nchini. Wakati kukiwa na ugumu huo, inaelezwa kuwa asilimia 70 ya Watanzania wanajishughulisha na kilimo, lakini wengi wanashindwa kufikia malengo kutokana na migogoro ya ardhi. Baadhi ya mipango ya Serikali ya kuinua uchumi ni pamoja na Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini (Mkukuta), Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara Tanzania (Mkurabita), Mkakati wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDS). Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP), Kilimo Kwanza, Uendelezaji Kilimo Ukanda wa Kusini Tanzania (SAGCOT), Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano ambao ulianza mwaka 2011-2016

Ukawa waanza kugawana Majimbo

Picha
Moshi. Baada ya kumalizika kwa Bunge la Katiba, hasira za Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) dhidi ya CCM zimehamia kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015, safari hii ukiunda kamati maalumu kutafuta namna ya kumsimamisha mgombea mmoja wa urais na kuachiana majimbo. Mwenyekiti mwenza wa Ukawa, James Mbatia ametoa maelezo hayo alipokuwa akizugumza na gazeti hili katika mahojiano maalumu hivi karibuni. Mbatia ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, alisema tayari kamati zimeundwa na zinaendelea na kazi ya kuratibu mpango huo mahususi, unaolenga kuiondoa CCM madarakani. “Lengo letu ni kuhakikisha Ukawa ina nguvu ya kushika dola katika Uchaguzi Mkuu wa 2015 na katika mpango huo, vyama vitaachiana majimbo na viti vya udiwani kulingana na nguvu ya chama katika sehemu husika,” alisema. Ukawa; umoja ulioanzishwa Februari mwaka huu ukiwa ni kikundi shinikizi katika mchakato wa Katiba katika siku za mwanzo za Bunge Maalumu la Katiba, unaundwa na vyama vya NCCR-Mageuzi, Chadema, C
Picha
Baadhi ya wananchi wakivuka Mto Maragalasi  upande wa Nchi ya Burundi kuingia Tanzania

DED Uyui apewa siku 60

W AZIRI Mkuu,Bw.Mizengo Pinda,amempa miezi miwili (siku60),Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, mkoa ni Tabora(DED),Bi,Khadija Makuani,kuhakikisha watumishi wote wilayani humo wawe wamehamia Isikizya yalipo Makao Makuu ya Wilaya hiyo . . Bw.Pinda alitoa agizo hilo juzi wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa Isikizya waliofika kushuhudia uzinduzi wa Makao Makuu ya Polisi wilayani humo. "DED nimekagua nyumba ya Mkuu wa Wilaya na kuzindua nyumba nane,miundombinu iliyopo inatosha,hamia we na watu wako,nataka ifikapo Desemba 31 mwaka huu,wote muwe Isikizya na ambaye atagoma,RC(Mkuu wa Mkoa), niletee jina lake. "Shauku ya wananchi kuwasubiri mhamie hapa imetosha,mtumishi ambaye atagoma niishara kuwa hataki kuwahudumia wananchi nasisitutasema hatukutaki...watumishi wengi wanajifanya wakubwamno kuliko wananchi mnaowahudumia," alisema Bw. Pinda. Bw. Pinda aliwasili Mjini Tabora juzi jioni nakutembelea Makao Makuu ya W

Lissu: Marehemu amepiga kura Katiba

MWANASHERIA wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu amesema mchakato wa kutengeneza katiba mpya ni wa kihistoria kwani jina la marehemu lilipiga kura. Akifafanua kauli hiyo alisema jina la mjumbe Shida Salum aliyefariki dunia Julai mwaka huu, limo kwenye orodha ya waliopiga kura ya ndiyo wakati kupitisha Katiba inayopendekezwa. Lissu alisema hayo mwishoni mwa wiki mjini hapa alipotoa mada kwenye mdahalo wa kujadili Katiba iliyopendekezwa inayosubiri kupigiwa kura na wananchi, ambako alihoji ni Katiba Mpya au katiba ya kiimla katika rangi ing’aayo. “Aliyekuwa mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba kundi la 201 kila mmoja anajua kwamba alifariki dunia lakini ukiangalia kwenye orodha ya waliopiga kura (huku akiionyesha kitabu kwa washiriki), anaonekana amepiga kura ya ndiyo. “…Hii inawezekanaje jamani, ndiyo maana nakubaliana na Rais (Jakaya Kikwete) kuwa hii katiba iliyopendekezwa ni ya kihistoria,” alisema Lissu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHAD

Zitto kung’oka CHADEMA

Picha
MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA), inadaiwa yupo katika hatua za mwisho kujiengua ndani ya chama hicho alichojijengea sifa kubwa Kwa mujibu wa watu walio karibu na Zitto, wamelidokeza Tanzania Daima Jumapili, kuwa mbunge huyo alipanga kujiondoa ndani ya chama hicho mwezi uliopita lakini alishindwa kufanya hivyo kwasababu ambazo hazijawekwa wazi. Inadaiwa Zitto, alipanga kuondoka CHADEMA sambamba na uzinduzi wa kitaifa wa chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania) uliopangwa ufanyike mwezi uliopita. Novemba 22, mwaka jana, Kamati Kuu ya CHADEMA iliamua kumvua nyadhifa za uongozi Zitto na wenzake wawili (Dk. Kitila Mkumbo na Samson Mwigamba) kwa madai ya kukisaliti na kukihujumu chama. Zitto alidaiwa kuwa kinara wa mkakati wa kuleta mabadiliko haramu ndani ya chama hicho, huku waasisi hao wakijipa majina ya MM, M1 na M2 ambao ndani yake anadaiwa kuwamo Dk.  Kitila Mkumbo, mjumbe wa CC na NEC. Hata hivyo Mkumbo na Mwigamba walivuliwa u

Ulaya wasikitishwa mchakato Katiba

UMOJA wa Ulaya (EU), umesikitishwa na Tanzania kutoitumia fursa ya uundwaji wa Katiba mpya kuiondoa adhabu ya kifo. EU, imeeleza hayo jana katika taarifa yake kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, ikiwa ni siku ya kupinga adhabu ya kifo na kueleza kuwa, itaendelea kupaza sauti hadi adhabu hiyo itakapofutwa. Pia, EU imeeleza kuwa Tanzania bado ina nafasi ya kuiondoa adhabu hiyo katika katiba pindi itakapopigiwa kura. EU na Baraza la Ulaya, limeeleza kuwa baada ya kutiliana saini na kuunganisha nguvu, watahakikisha wanaendelea kupinga adhabu hiyo katika kesi zote ili dunia iikomeshe na kulinda ulinzi wa haki za binadamu. Umoja huo umeeleza kuwa jumuiya hiyo italinda na kuhakikisha hakuna mwanachama anayetumia adhabu hiyo na kuleza kuwa mwaka huu idadi ya watu waliohukumiwa adhabu hiyo imeongezeka. Aidha, EU imetoa wito kwa kwa nchi za Afrika kuendelea kukubali itifaki na mikataba ya kutetea haki za binadamu na kukomeshwa adhabu. Pia, EU iliyapongeza mashirika mb