Serikali yafunga migodi ya machimbo ya Dhahabu

Issa Machibya mkuu wa mkoa wa kigoma alipokuwa akiongea na wananchi wa kijiji cha kinyinya wilayani kakonko alipotoa amri ya kufunga migodi ya dhaabu


Wananchi wa kijiji cha kinyinya wakiwa mkutanoni
Kamati ya ulinzi usalama kigoma wakiwa ktk mkutano wa hadhara katika kijiji cha kinyinya  kwa ajili ya kuona namna ya kutatua migogoro ya wakulima na wafugaji
Serikali yafunga migodi ya machimbo ya Dhah
abu



Serikali imeamulu kufungwa kwa migodi yote ya machimbo ya Dhaabu iliyoko katika kata ya Nyamtukuza  wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma

Amri imetolewa  na mkuu wa mkoa huo Issa Machibya alipokuwa akiongea na wananchi wa Kijiji cha Kinyinya wilayani humo kwenye mkutano wa hadhara alipokwenda kujionea hali halisi ilivyo baada ya kutokea mapigano ya wakulima wakigombea ardhi hatua iliyopelekea jumla ya watu watatu kupoteza maisha katika maeneo ya mashambani

Uamzi huo umekuja baada ya wakazi wa wakijiji hicho kutoa maelezo yao kuwa chanzo cha vulugu ni ni migodi hisiyokuwa rasmi inayokusanya watu kutoka sehemu mbalimbali ambapo watu wengi waliingi katika vijiji vya Tarafa hiyo na baadae wageni hao kuamua kujichukulia ardhi na kuingiza mifugo bila utaratibu na sheria. na baadae kusababisha vitendo vya ujambazi na kugombania ardhi



Aidha wakazi hao wameomba serikali kushugulikia matatizo hayo, ikizingatiwa wakati huu ni msimu wa kilimo, kwani hivi sasa hawawezi kwenda mashambani kuendelea na kazi zao za kilimo kwa kuhofia kuvamiwa na waakulima wenzao na kufanyiwa vitendo vya kikatili kupigwa viboko na kujeruhiwa  kunyang’nywa mali zao

Wamesema kuwa wapo baadhi ya jamaa zao ambahawajulikani walipo baada ya kuanza kuvamiwa na watu waliowataja kuwa ni wasukuma na kufanyiwa vurugu


Pamoja na mambo mengine wakazi hao wameendelea kuushutumu uongozi wa kijiji hicho kwa kutofuata taratibu na sheria kwa kuwakaribisha wageni bila kuwashirikisha wananchi katika mikutano ya kijiji bali wao uenda kukusanya hela kwa wakulima na wafugaji wanaohamia katika kijiji hicho  hali inayoleta usumbufu kwa wenyeji kwa kuchukulia ardhi zao na kulishiwa mifugo kwenye mashamba yao ambapo wanapopeleka malalamiko katika uongozi wa kijiji hayafanyiwi kazi



Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha kinyinya Justin Kilegea alikanusha tuhuma zilzoelekezwa kwake na kusema hela zilizowahi kuchangishwa kwa wakulima wahamiaji ni zilikuwa kwa ajili ya kuendeleza benki ya Matofari ya kijiji, ila mgogoro ulitokea baada ya ya mfugaji kuuwa na ng’ombe wake kukatwakatwa na watu wasiyojulikana


Mkuu  wa mkoa huo alitoa wito kuwa watanzania wote wanatakiwa kuthaminiana kwakuwa katika nchi hii hakuna mambo ya kikabila na kila mtu ana haki ya kuishi maali popote bali afuate taratibu na sheria na kuutaka uongozi wa kijiji na kata hiyo kuhamasisha amani katika jamii


Machibya alitoa amri ya kufunga migodi yote ya dhaabu Kanyomvi, Nyamwilonge Lutela na mingine  ilioanza zamani naya karibuni ili utaratibu unaokubalika uweze kufanyika na watu woe waishi kwa Amani


Wahamiaji hao wanatajwa kuwa waliingia katika maeneo hayo kwa kufuata madini na ufugaji kasha baadae kuchukua ardhi na kuanza kulima hali iliyopelekea ugomvi wa ardhi

Hatua hiyo imekuja baada ya mfugaji mmoja kuuwawa na watu wasiyojulikana na Ng’ombe wake kutwakatwa na mapanga na baadhi ya wakulima na wafugaji wanaotajwa kutoka katika mikoa ya Mwanza na shinyanga kuamua klipiza kisasi na kuwauwa wakulima wenyeji wawili na wengine kadhaa kupotea.




Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao