Watu wawili wafa katika mapigano kugombania ardhi na ukabila


Wananchi wa kijiji cha Kinyinya wakimsikiliza Dc
Askali Polis wilaya ya Kakonko waliokuwa wanalinda usalama wakati wa mapigano kati ya wakulima Waha na Wasukuma Kijiji cha kinyinya na Kakonko ambapo watu waili walipoteza maisha
Venance Mwamoto kaimu mkuu wa wilaya ya kakonkoalopokuwaakizungumza na wakazi wa kijiji cha kinyinya Tarafa ya Nyaronga Kakonko wakati wa vurugu za kugombea ardhi kati ya wasukuma na waha


Watu wawili wafa katika mapigano kugombania ardhi na ukabila
Nyumba ya mkulima kijiji cha Kinyinya kakonko


Watu wawili wamekufa na wengine hawajulikani walipo baada ya kuzuka mapigano kwa ajili ya kugombania ardhi kati ya kabila la Wasukuma na Waha  katika kijiji cha kinyinya  kata ya nyamtukuza wilaya ya Kakonko mkoa wa Kigoma

 Mwenyekiti wa kijiji hicho Bw Justini Kilegea, amesema kuwa  mapigano hayo yamewahusisha watu wa kabila la Wasukuma dhidi ya kabila la Waha  usiku wa kuamkia jana baada watu wa kabila la  wasukuma wanaoishi mashambani  kuvamia nyumba za   waha na kuawapiga kwa madai kuwa wanatakiwa wa waambie majambazi  wanaishi wapi nakuanza kuzusha vurugu kwa kuchoma nyumba na kuuwa watu wawili na wengine hajulikani walipo 

Hata hivyo amedai kuwa mapigano hayo yamehusishwa na  swala la ulipzaji kisasa baada ya tar 15oktoba 2014 watu wasiyojulikana kumuua mtu mmoja wa kabila la wasukuma na kutakata Ng’ombe  wake kwenye maeneo hayo ya mashambani ndipo nao wasukuma walipoamua kulipiza kisasi kwa kuwavamia Waha na kusababisha mauwaji ya waliouwa ni Kachila Kahegele umri miaka 48 na Lamecki Kachila miaka 26 wate wanaume.


Nae Kaimu mkuu wa wilaya hiyo Venance Mwamoto na kamati ya ulinzi usalama walifika katika kijiji hicho na kuwataka wananchi kuacha kushambuliana na kulipiza visasi kwani hali hiyo ni hatari sana kwani inaweza kuleta vurugu zisizoisha, baada ya kusikia kuwa Watu wa kabila la waha nao wameamua kwenda katika maeneo hayo kwa ajili ya kulipiza kisasi juu ya ndugu zao waliokufa na wengine kupotea


Aidha Mwamoto amewata wanasiasa kutoliingilia swala hilo kisisa  kwani wote wanatakiwa kushirikiana kuweza kutatua matatizo yao ili jamii iishi kwa Amani na utulivu

Amesema kuwa kila mtu anaruhusiwa kuishi maali popote hapa nchini isipokuwa anapotaka kwendakuishi katika kijiji chochote lazima auone uongozi husika na wananchi washirikishwe kwa njia ya mikutano ya hadhara juu ya mtu anayeingia katika eneo lao


Kwa upande wao baadhi ya wakazi wa kijiji hicho, wamesema kuwa mgogoro huo ni wa siku nyingi kati ya wasukuma na waha wanaoishi mashambani wakigombania ardhi 


Aidha wakazi hao wameulalamikia uongozi wa kijiji hicho kwa kulifumbia macho swala hilo hadi kufikia hatua hiyo kwani wamekuwa wakiwaeleza mara kwa mara maana wapo baadhi ya watu  kama wafugaji wamekuwa wakiingia katika  kijiji hicho na kuchukua ardhi  nguvu bila utaratibu

Wamesema kuwa wageni wengi hususa ni wafugaji wamekuwa wakimilikishwa maeneo bila kuwa shirikisha wananchi hali ambayo imekuwa ikisababisha mvutano mkubwa kati yao na wageni hao  

Mwenyekiti wa kijiji hicho alipoulizwa juu ya tuhuma zinazo mkabili yeye na wenzake kuwa wao ndiyo wanosababisha mgogoro huo kuwa mkubwa kwa kuufubia macho kwa kugawa ardhi ya kijiji bila utaratibu na sheria   kwa kutowashirikisha wananchi katika mikutano ya kijiji  alikana tuhuma hizo na kudai kuwa yeye alipoingia madarakani aliwakuta hivyo hajui waliingiaje hapo kijijini na wanajitahitadi kulishugulikia swala hilo ili aman iwepo



Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao