ALATI MKOA WA KIGOMA WAKAGUA MIRADI KIBONDO

 Jumuiya ya Serikali za Mitaa Tanzania ALATI Mkoa wa Kigoma imeishauri Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma kuboresha mazingira ya ujifunzaji kwa Wanafunzi wa Chuo cha Maafisa Matabibu kinachomilikiwa na Halmashauri hiyo

Wametoa ushauri huo Wajumbe wa Jumuiya hiyo wakiwa kwenye ziara ya kutembelea na kukagua Miradi ambapo wameeleza kulingana na uhimu wa sekta ya afya ni vema uboreshajiwa miundombinu katika chuo hicho ufanyike haraka iwezekanavyo

Hatua hiyo imekuja baada ya kupokea taarifa ya namna chuo hicho kinavyoendeshwa na kutoa huduma ambapo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Kibondo Diocles Lutema  ameeleza kwakuwa chuo hicho kinamilikiwa na serikali wanafuata miongozo

Miradi iliyotembelewa na Jumuiya hiyo ni Ujenzi wa Soko la Kisasa, Chuo cha maafisa Tabibu, Jengo la Ofisi za Halmashauri ya Kibondo na Vibanda vya Biashara, huku  baadhi ya ambao ni Lugendo Elias na Anthon Kiteleriwajumbe hao wakipongeza ujenzi wa Miradi hiyo huku nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kibondo

 Mwenyekiti wa Alati Mkoa wa Kigoma ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kibondo  Alex Baragomwa wakati wa kuhitimisha ziara hiyo amepongeza maoni na ushauri wa wajumbe wa Jumuiya hiyo huku  akiahidi kutekeleza ushauri na maelekezo hayo yaliyotolewa




Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI SGR NA KUZINDUA MELI NNE ZA MIZIGO ZIWA TANGANYIKA

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu