DC MAGU AZITAKA MAMLAKA ZINAZOZOJIHUSISHA NA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA KUFANYA KAZI KABLA YA MVUA KUNYESHA
Katika
kukabiliana na Matatizo ya Mvua kubwa ziilizotabiriwa na Mamlaka ya hali ya
Hewa nchini TMA , Mkuu wa Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza Jubileti Lauwo,amezitaka
Mamlaka zote zinazohusika kukabiliana na
majanga kufanya utekelezaji kazi husika
kwa wakati kabla Mvua hizo hazijaanza kunyesha
Akiongea
mara baada ya Kikao na Viongozi kuanzia
ngazi za Vijiji na Wataalam mbalimbali amesema ameziagiza Mamlaka zinazohusika
na Miundo mbinu ya Barabara yaani Wakala wa huduma za Barabara za Mijini
Vijijini TARURA na TANROAD kuboresha miundombinu hiyo haraka kwani ni muhimu
kwa Maisha ya Watu
Aidha amesistiza mikataba inayotajwa kuhakisha inafanyiwa kazi maana Mvua zinatarajiwa kunyesha siku si nyingi zijazo kwa hiyo ni vema Barabara zote zikawa zimeimarishwa mapema na kurekebisha njia za Maji
![]() |
| Jubileti Lauwo Mkuu wa Wilaya ya Magu akiwa kwenye Kikao na Viongozi Wilayani Magu wakijadili namna kuchukua tahadhari ya Elinino |
Hata hivyo Jubileti amesema katikaWilaya yakewamejipanga kuhakikisha hayatokei Majanga iwapo kama Mvua zitanyesha nabado wanaendelea kuwaelimisha Wananchi kuhusu Mvua za Elinino
Baadhi ya
washiriki wa Kikao hicho , wakatoa ushauri wao juu ya kuimarisha Barabara kwa
TANROAD NA TARURA huku Mwakilishi wa TANROAD Mkoa wa Mwanza Ramadhani Majaliwa
akieleza kuwa wameshaanza utekelezaji kuhakikisha Barabara zinapitika muda wote
Kwa kuwa
Mvua hizo zinatarajiwa huenda zikaanza kunyesha mwishoni mwa mwezi Septemba au
mwanzo ni mwa Oktoba, ushauri ukatolewa juu ya suala la utoaji taarifa za
haraka iwapo linatokea jambo kwa ajili ya msaada wa haraka ameeleza Kaimu
Mkurugenzi Halmashauri ya Magu Mohamed Kyando
Kwa kuwa
Mvua hizo zinatarajiwa huenda zikaanza kunyesha mwishoni mwa mwezi Septemba au
mwanzo ni mwa Oktoba, ushauri ukatolewa juu ya suala la utoaji taarifa za
haraka iwapo linatokea jambo kwa ajili ya msaada wa haraka ameeleza Kaimu
Mkurugenzi Halmashauri ya Magu Mohamed Kyando



Maoni
Chapisha Maoni