Kugombea pamoja si uadui bali tushikiane ili kuijenga Tanzania ijayo

Wanaotarajiwa kuingia katika kinyang,anyiro cha  uchaguzi mkuu hapa nchini kuwani viti mbalimbali vya ubunge Udiwani na Urais wametakiwa kujenga umoja kwa wananchi wanaotakiwa kuwapigia kura pasipo kuwagawa  na kusababisha hali ambazo hazistaili katika Taifa

Akiongea kwenye mkutano wa adhara mjini kibondo mkoa wa kigoma mbunge anemaliza muda wake Felix Mkosamali amsema kuwa kuwa kitendo cha kugombea au kutafuta nafasi moja mkiwa wengi si uaduai hata kama kuna itikadi tofauti za vyama bali kila mgombea anatakiwa kutambua kuwa hii nchi ni mali ya watanzania wote na kinachotakiwa ni kuacha malumbano

Amesema kuwa hali hiyo ya mgawanyiko inayowakumba wengi na kuamua kuwaingizia wafuasi wao mambo yanayoweza kusababisha vurugu na kuvunja undugu hatua inayoonyesha taswila ya kutokomaa kwa siasa katika Tanzania na Bara la Afrika

Mkosamali katika mkutano amejiata kuwa nae mwaka huu amechukua fom ya kugombea Ubunge katika Jimbo la Muhambwe kupitia umoja wa katiba ya wananchi Ukawa kupitia chama cha NCCR Mageuzi 

Kutokana na ahli hiyo amewataka wananchi wa Kibondo kufanya kampeni zenye ustarabu hasa kilenga na kutarajia matokeo mazuri baada ya uchaguzi na ktika kuliendeleza Taifa maana maana watanzani wengi wanakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinawapelekea kuhitaji viongozi mahili na wazalendo

Nae Afisa uchaguzi Jimbo la Buyungu Bw, Adam. A. Adam amefafanua kuwa watanzania wengi hawana elimu ya kuendesha kampeni na namna ya upigaji kura hali inayowapelekea wengi kujikuta wameingia katika mikono ya sheria kwa kwenda kinyume na taratibu na kuwataka wagombea wote kuwaelimisha wafuasi wao kwani wenyewe upewa maelekezo ya kuendesha kampeni

Aidha ameongeza kusema kuwa muda wa vyama vyote kutoa matangazo ya kampeni nikuanzia saa kumi na mbili jioni hadi saa mbili usiku na kuelekeza kuwa chama chochote hakitakiwi kutoa matangazo yake kabla na baada ya muda huo na kuda kuwa wataendelea kuelekezana na viongozi na kuonyana kabla ya kuchukua hatua za kisheria ila atakaeonyesha kuendelea kukiuka utaratibu hatua zaidi zitachukuliwa

Felix Mkosamali mbunge anaemaliza muda wake Jimbo la Buyungu
 
Wananchi wa Kibondo  wakimsikiliza mbunge anaemaliza muda wake Felix Mkosamali kwenye mkutano wa hadhara
 Mbunge anayemaliza muda wake Mkosamali

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao