Watakiwa kusalimisha Siraha Haramu kwa muda uliopangwa

Watakiwa kusalimisha Siraha Haramu  kwa muda uliopangwa


Mrakibu wa Polis  Marko Joshua Ocd Kibondo

Katika hatua ya kuboresha hali ya usalama hapa nchini,Jeshi la Polisi kuanzia june 12 mwaka huu lilitoa muda  wa kusalimisha siraha haramu kwa iyali zinazomilikiwa kinyume cha sheria

Mkuu wa Polis wa wilaya kibondo mkoani kigoma Marko Joshua alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana,  ameitaka jamii kuutumia vizuri muda uliotolewa na serikali kwa  kuhakikisha kila mtu anayemiliki siraha yoyote kinyume cha sheria anaisalimisha ili kudumisha dhana ya kutii wa sheria bila shuluti na kuongeza kuwa mtu anaweza kupeleka katika ofisi ya kata au kijiji au kituo chochote cha polisi na asisumbuliwe

Joshua amesema kuwa muda uliotolewa na serikali ni kuazia june 12 hadi september 12 mwaka huu, kwa yule ambaye  hatafuata utaratibu huo,  kutapitika msako mkali ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua kali za kisheria wale watakao bainika kwani mpaka sasa hakuna siraha iliyokwisha salimishwa na kuwataka viongozi wa dini kuwaelimisha waumini wao, madhala ya kumiliki siraha haramu

Siraha haramu zinatajwa kutumika katika vitendo vya uharifu kama ujambazi, uwindaji haramu, kwenye mapori ya akiba na hifadhi za Taifa na utekeji wa magari huku, mtendaji wa kijiji cha kagezi  Kazala Dama,s akieleza kuwa katika kijiji chake hakuna mtu aliyekwisha salimisha siraha na kuda kudai kwa hivi sasa hali simbaya sana ikilinganishwa na siku zilizopita watu walikuwa wakivamiwa na kunyang’anywa mali zao hasa maeneo ya mipakani

Laurence Kagina ni mkazi wa kijiji cha Kibuye kilichoko mpakani mwa Tanzania na Burundi yeye anasema kuwa baada ya seikali kuweka vituo vya polisi karibu na vijiji vya mpakani na katikati hali imekuwa nzuri  maana waarifu wamekuwa wakishirikiana watu kutoka Burundi na kuwavamia watanzania na kuwanyang;anya mali zao na kusababisha hata vifo

Aidha wakazi wa maeneo ya kibondo wameiomba serikali kuendelea kutoa elimu juu ya umiliki wa siraha haramu kwani hatari sana zinapoendelea kuwemo miongoni mwa jamii kama alivyoeleza Tahabiti Yusuph mkazi  wa Kigina huku mchungaji wa kanisa la T.A.G Emmanuel Koreshi akisistiza kutolewa maelekezo kwa makundi tofauti kwani elimu na ujumbe haujaifikia jamii inavyotakiwa maana yeye hajasikia kama kuna iliyosalimishwa

Katika mkoa wa Kigoma kumekuwa kuwa kukiripotiwa vitendo vya uharifu wa kutumia siraha vinavyosadikiwa kuwa vinafanywa na majambazi vijijini huku baadhi ya wananchi wakiwashutumu wakimbizi wanaohifadhiwa hapa nchini kwa kukimbia machafuko katika nchi zao na wengine kutoka katika nchi mojakwamoja na kushirikiana na wenyeji wa Tanzania kwasababu mkoa  huo unapakana na nchi za Burundi na Kongo
Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao