Vijana hapa nchi wametakiwa kujitambua kuwa wao ni kundi muhimu sana na linalotegemewa kama nguvu kazi ya Taifa, hivyo kutokana na hali hiyo wasikubali kutumiwa vibaya katika jambo lilote hasa katika kipindi hiki cha kampen za kuelekea uchaguzi mkuu oktoba 25 mwaka huu

Vijana wametakiwa kujitambua


Vijana  hapa nchi wametakiwa kujitambua kuwa  wao ni kundi muhimu sana na linalotegemewa  kama nguvu kazi ya Taifa, hivyo kutokana na hali hiyo wasikubali kutumiwa vibaya katika jambo lilote hasa katika kipindi hiki cha kampen za kuelekea uchaguzi mkuu oktoba 25 mwaka huu

Akiongea kwenye mkutanu wa uzinduzi wa  kampeni za chama cha mapinduzi uliofanyika katika Tarafa ya kifura wilaya kibondo mkoani Kigoma, aliyekuwa mgombea Ubunge kura za maoni kisha kuengeliwa na halmashauri kuu ya Ccm, Jamal Abdalah amesema kuwa vijana wengi hawajaweza kujitambu umuhimu walionao hali inayopelekea kurubuniwa na kujiingiza katika vitendo visivyostaili

Jamal aliyekuwa mshindi katika kura za maoni na kuondolewa katika nafasi hiyo, amezidi kumnadi mgombea aliyepata nafasi ya tatu  na baadae kuteuliwa kuwa mgombea ubunge jimbo la Muhambwe Atashasta Nditiye amewataka wanachama  wa ccm na vyama vingine hususa vijana kutokubali kutumiwa vibaya katika uchaguzi 2015 na kuacha makundi wao wafanye maamuzi mema


Uzinduzi wa kampeni hizo ccm zilitaka kuingiwa na dosari baada ya baadhi  vijana ambao hawakufahamika majina yao kwa haraka kutajwa kuwa walitaka kuleta vurugu na kuanza kurushiana maneno na katibu wa chama hicho Bw, Hamis Kananda na baadae gasia hizo kuzimwa


Kampeni hizo zilizozinduliwa jana kote nchini, kwa upande wa jimbo la Muhambwe  umoja wa katiba ya wananchi ukawa waliendesha mkutano wao katika kata ya Kibondo mjini,  ACT Wazalendo haijafahamika watazindua lini, kwa kumnadi mgombea wao Bw Edgar Mkosamali wakati Chama cha Chauma kimeandaa kuzindua kampeni zao jumatano wiki hii kikiwakilishwa na Nduilabusa mapigano,  huku wagombea ubunge wa Ccm na Ukawa kupitia NCCR Mageuzi ambao ni Atashasta Nditiye na Felix Mkosamali wakijinadi kwa ahadi mbalimbali

Kampeni hizo ilizoanza jana Agast 22 ni kwa ajili ya kuwanadi wagaombea  urais, Ubunge na Udiwani kwa vyama vyote vya siasa hapa nchi kuelekea uchaguzi mkuu ambapo watanzania wote wanatakiwa kuwa watulivu waadilifu na kuchukua maamuzi yenye tija kwa ajili ya uendelevu wa taifa lao bila kufuata ushabiki wotewote kwa kukumbuka kuilinda Amani ya nchi hii kwani imo mikononi mwao wenyewe  


Mwisho
Felix Mkosamali mgombea ubunge jimbo la Muhambwe 2015

Wananchi wakimsikiliza mgombea ubunge mjini kibondo

Add caption

Wananchi na wanachama wa ccm wakiwa kwenye kampen za uchaguzi 

Jamal Abdalah aliyeengeliwa na NEC akimnadi mwenzake katika mkutano wa kampeni

Atashasta Nditiye mgombea ubunge jimbo la Muhambwe 2015

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao