Pongezi kwa Issa Machaibya RC Kigoma, kwa kutoa msahada wa chakula na vifaa vya ujenzi katika shule



Ili jamii hapa nchini iweze kuwa na moyo wa kujitolea katika shuguli za maendeleo inatakiwa kuwepo na ushirikishwaji wa dhati kati ya viongozi na wananchi ikiwemo motisha hasa pale inapothibitika baadhi yao  wameitikia wito na kushiriki katika kazi za maendeleo ndani ya jamii. 

Mkuu wa mkoa wa Kigoma Issa Machibya, ametoa vifaa vya ujenzi na chakula kwa ajili ya shule sekondari Mugombe iliyoko katika Kata ya Kagezi wilani kibondo, ikiwa ni motisha baada ya kukuta wamepiga hatua katika ujenzi wa Maabara

Akikabidhi vitu hivyo jana, kwa niaba ya mkuu huyo wa mkoa katibu tawala wa wilaya kibondo Ayubu Sebabili, kwa Afisa elimu shule za sekondari Bi Honorata Kabundugulu, amesema kuwa hiyo ni ahadi aliyoitoa wakati alipokwenda katika ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa maabara na kukuta wamepiga hatua kubwa shuleni hapo.

Aidha amesema kuwa zawadi  hiyo ni vizuri ukatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na kueleza kwa ni kwa ajili ya kuwahamasisha wananchi kushiriki katika shuguli za maendeleo na kutaja vitu hivyo kuwa ni pamoja na Mifuko 30 ya saruji, Sukari kilo mia 1 na mifuko 25 ya unga wa sembe kwa ajili ya wanafunzi kupata chakula shuleni, vyenye thamani Tsh million 2  

   Nae Bi Honorata Kabundugulu alipokuwa akipokea zawadi hizo, amepongeza uamuzi  wa mkuu wa mkoa kwani utaongeza ushawishi wa kushiriki kwa wananchi na watumishi wengine kwenye shuguli za maendeleo huku mkuu wa shule hiyo Tanu Selemani akishukuru kwa kuwa ahadi hiyo iliahidiwa na kutekelezwa na kudai kuwa si kwamba wao ni wazuri sana kuliko wengine katika utendaji

Kwa upande wao wanafunzi wa shule ya sekondari ya kumwambu wasema kuwa mkuu huyo wa mkoa amefanya vema kuonyesha  mfano wa kuchangia chakula katika shuleni ya wenzao, kwani swala hilo limekuwa ni gumu kwa wazazi wengi, hatua inayosababisha wanafunzi kushiriki masomo kwa shida mara wanapohisi njaa



Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao