Wakazi wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma wameitaka serikali ijayo kuhakikisha inatatua kero zinazowakabili wananchi katika maeneo mengi hapa nchini hususa kwa wale wanaoishi vijijini ambao kufikiwa na huduma mbalimbali za kijamii ni kwa kususua



Aisha Meda mkazi wa kiyobelas

Juma Maganga mgombea udiwani kakonko

Caros Gwamagobe aliyekuwa mgombea ubunge kura za maoni ccm Buyungu

Christopha Chiiza mgombea ubunge Buyungu akipokea Ilani ya chama cha mapinduzi

Julias Mbwiga katibu Ccm Kakonko 



Mwinyi Ramadhani mkazi wa kakonko
Wakazi wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma wameitaka serikali ijayo kuhakikisha inatatua kero zinazowakabili wananchi katika maeneo mengi hapa nchini hususa kwa wale wanaoishi vijijini ambao  kufikiwa na huduma mbalimbali za kijamii  ni kwa kususua

Wakiongea na clouds Tv wananchi hao ambao ni Ramadhan Mwinyi, Aisha Medas na Juliana Emily, wamesema kuwa hivi wananchi wanakumbwa na matatizo mengi ikiwa ni kukosa huduma za Afya, Maji, Barabara na Elimu na hata kutotendewa haki na baadhi ya viongozi wa ngazi za vijiji na kata hatua inayokwamisha juhudi za maendeleo

Wameeleza kuwa hivi sasa nchi inaelekea kipindi cha uchaguzi mkuu wagombea wengi wa wanafasi za Urais, Ubunge na Udiwani, wanapita na kutoa ahadi nyingi kwa wananchi hivyo ahadi hizo kwa wale watakaopata lidhaa  hawana budi kuzitimiza kwani kinyume chake ni kuwakatisha tamaa wananchi

Hata hivyo katika kuzindua wa  kampen za uchaguzi ccm Jimbo la Buyungu wilayani humo, katika harakati za kuwanadi wagombea wake,  Katibu wa chama hicho Julias Mbwiga amesema kuwa ziko changamo hasa katika kukamilisha miundo mbinu ya maji lakini wamejipanga kuzimaliza kipindi kinachofuata sasa

Kwa upande wake Waziri wa Uwekezaji na uwezeshaji ambaye pia ni mgombea ubunge jimbo hilo la Buyungu, amesema kuwa yeye atatumia ilani ya chama hicho japo lipo tatizo la matumizi mabaya ya fedha za serikali zinazotolewa kwa ajili ya huduma mbalimbali kupitia katika halmashauri ya wilaya akaahidi kusimamia ili mafanikio yawepo

Jimbo hilo kupitia vyama mbalimbali lina wagombea wa nafasi za ubunge watatu ikiwa ni Metusela Atanas NCCR Mageuzi, Samson Bilago CHADEMA na Christopha Chiiza kupitia CCM



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao