Shule ya msingi Nengo ya Walemavu, iliyoko wilayani Kibondo mkoani kigoma, inayohudumia wanafunzi walemavu wa mahitaji maalum inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni ukosefu wa maji Vifaa vya kujinfunza na kufundishia na vyombo vya kulia chakula



Wanafunzi shule ya msingi Nengo elimu maalum walemavu
Elisha  George mwanafunzi shule ya msingi nengo walemavu 

Lukas Frand muu wa shule ya Nengo



Islafil Ntoteye mwenyekiti chama cha walemavu wa ngozi w kibondo


Shule ya msingi Nengo iliyoko wilayani Kibondo mkoani kigoma, inayohudumia wanafunzi walemavu wa mahitaji maalum inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni ukosefu wa maji  Vifaa vya kujinfunza na kufundishia na vyombo vya kulia chakula

Akisoma lisara kwa niaba ya wanafunzi wenzake wakati wa afla ya matembezi kwa ajili ya kutoa elimu juu ya kuwatambua na kuwa thamini walemavu yaliyoandaliwa chama cha walemavu wa ngozi Tas kwa kuzishirikisha  baadhi ya shule za sekondari za  mjini kibondo Elisha George ambaye ni mlemavu wa macho, hali inayoweza kusababisha kiwango cha elimu kushuka

Ameeleza kuwa  kwa wanafunzi ambao si walemavu wa viungo wanatumia muda mrefu kuchota maji badala ya kusoma, kwa ajili ya kuwasaidia wenzao  wasiyokuwa na uwezo kulingana na viwango vya ulemavu walivyonavyo

  Hata hivyo wameongeza kuwa wakati wa kupata chakula hawezi kupata chakula hicho kwa pamoja kwasababu ya ukosefu wa vyombo hali ambayo uwalazimu kubiliana huku wakiiomba serikali kulitazama swala hilo na kuomba kupatiwa vitabu kwa ajili ya kujifunzia vikimo  vya nukta nundu kwa wasioona

Mkuu wa shule hiyo Bw Lukas Frandy amesema kuwa fedha inayotolewa kuendesha shule hiyo ni kidogo sana kulingana  na hali za watoto wenyewe na wengine uri wao ni mdogo sana ulio chini ya miaka mitano na kudai tatizo kuwa ni jamii kubwa hapa nchini, inakosa elimu mahususi ya kuwatambua na kuwathamini watato walemavu kuwa hata wao wanaweza hali inayoonekana

Pamoja na mambo mengine mwenyekiti wa chama cha walemavu wa Ngozi Tas wilaya kibondo Bw, Islafil Ntoteye  katika taarifa yake kwa jamii amesema kuwa kwa upande wa walemavu wa ngozi kuwa  hiyo ni hali ya kawaida kwa binadamu  kukosa vinasaba ambavyo upelekea kuzaliwa mtu Albino kuitaka jamii kuachana na tabia kuwaita Dill, Biashara au Zeruzeru, huku Filbert Misuzi ambaye alimwakilisha mkurugenzi wa Halmashauri akiitaka jamii kupeleka watoto shule ili waelimike na kuondokana na dhana potovfu za ushirikina

Akijibu lisara hiyo mwakilishi wa mkuu wa wilaya kibondo ambae alikuwa mgeni rasmi katika sherhr hiyo, mkaguzi wa jeshi la  Polisi Tanzani Fotunatus Fransis amesema kuwa matatizo hayo atayafikisha kwenye ofisi husika, na kulingana hali hiyo ya kuwindwa kwa kundi la walemavu wa ngozi amesema jeshi hilo linaadaa mpango wa kuwa wanakutana wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ili kutoa elimu juu ya ulinzi shirikishi

Kasim Fatilo afisa elimu maalum amesema  vifaa vya kufundishia katika elimu maalum ni bei kubwa hivyo wamefanya utaratibu kuomba wizara ya elimu, na upande wa maji ameeleza kuwa maji yanapo katika ndo wanafunzi wengine ulazimika kuchata maji kwa ajili ya matumizi

Shule zilizoshiriki katika matembezi hayo ni Bishop mpango sekondari, Tutuba , shule ya sekondari ya wasichana kibondo, na Mount Chanza sekondari


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao