Wizara ya Viwanda kushirikiana na Taasisi zingine zenye nia ya kuanzisha Biashara
Wizara ya Viwanda na
Biashara imesema itaendelea kushirikiana na taasisi nyingine za serikali kuweka
mazingira rafiki kwa wale wote wenye nia ya kuanzisha biashara katika mkoa wa
Kigoma, wanafanikiwa kufanya hivyo kwa kuwapatia motisha na upendeleo maalum ambao
upo kisheria.
Hayo yameelezwa na
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Dennis Londo, wakati akifungua Maonyesho ya
Kimataifa ya Biashara (Lake Tanganyika International Expo 2026), yanafanyika
katika viwanja vya Mwanga Community Center mkoani Kigoma kwa kauli mbiu isemayo
‘Kigoma ni Kisima cha Fursa na Uwekezaji’.
Mkuu wa Wilaya ya
Kigoma Dkt. Rashid Chuachua, ambaye amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwenye
ufunguzi wa maonyesho hayo, amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kuweka
mazingira wezeshi ya biashara na uwekezaji.
Balozi wa Ubalozi
Mdogo wa Burundi mkoani Kigoma, Kekenwa Jeremiah, amesema maonyesho ya biashara
ni zaidi ya mahali pa kufanyia miamala ya fedha bali mahali ambapo tamaduni
hukutana na mawazo huungana ili kuchochea maendeleo, huku Katibu Tawala wa Mkoa
wa Kigoma Ndg. Hassan Rugwa akiwataka wafanyabiashara kuchangamkia fursa za
kibiashara zilizopo Kigoma.
.





Maoni
Chapisha Maoni