Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2014

Mahakamani kwa kujifanya Afisa wa usalama wa Taifa

Mahakamani kwa kujifanya Afisa wa usalama wa Taifa Mkazi wa Kinyerezi jijini Dar es salaam amehukumiwa kifungo cha miezi 24 jela au faini ya shilingi laki moja na nusu katika mahakama ya wilaya ya kibondo mkoa wa kigoma, baada ya kukili makaosa ya kujifanya mtumishi wa serikali wa jeshi la wananchi Tanzania na kujifanya afisa usalama wa taifa   Mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya kibondo bw Erick Marley mwendesha mashitaka wa polisi bw Frank Ruvanda amemtaja mtu huyo kuwa ni Wiston Ezekiel Bulinjie mwenye umri wa miaka 38 mkazi wa kinyerezi dar es salaam Bw Ruvanda amesema kuwa mnamo Agost 12 mwaka huu majira ya saa 9 alasiri bw Bulinjie alikwenda kikosi cha 824 KJ kanembwa Jkt wilayani kakonko alijitambulisha kwa Erast Sebasitian Tesha kuwa yeye ni askari wa jeshi la wananchi Tanzania kitu ambacho hakikuwa cha kweli , tarehe hiyo hiyo majira ya saa11 jioni akiwa kibondo mjini alijitambulisha kwa Godifrey Mpigwa kuwa yeye ni afisa usalama wa taifa Kesi

Mahakamani kwa kusababisha kifo kwa kumpa muwa unaosadikiwa kuwa na sumu

Mahakamani kwa kusababisha kifo kwa kumpa muwa unaosadikiwa kuwa na sumu Mkazi wa kijiji cha kumsenga wilayani kibondo mkoani kigoma amefikishwa katika mahakama ya wilaya ya kibondo kwa tuhuma za mauaji ambapo inasadikika kuwa alimpa muwa wenye sumu bw Matane Ndegea na kusababisha kifo chake Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya kibondo bw Mulokozi Kamuntu mwendesha mashitaka wa polisi bw Frank Ruvanda amemtaja mtu huyo kuwa ni Sintegeza Ally mwenye umri wa miaka 38 mkazi wa kijiji cha kumsenga Bw Ruvanda amesema kuwa mnamo September 08 mwaka huu majira ya saa tisa alasiri bw Sintegeza ally  kwa makusudi alimuua  bw Matane Ndegea kwa kumpa muwa wenye sumu ambao ulipelekea kifo chake Hakimu mkazi bw Kamuntu ameahilisha kesi hiyo mpaka itakapotajwa tena September 30 mwaka huu na mshitakiwa hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauji hivyo mshitakiwa yuko rumande kutokana na kwamba kesi yake haina mdhamana  Mwish

SERIKALI KUVIHAKIKI VYAMA VYA KIJAMII

SERIKALI imedhamiria kuanza mchakato wa kuhakiki vyama vya kijamii ili kuboresha huduma zinazotolewa na vyama hivyo nchini tangu kuanzishwa kwake. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bw. Isack Nantanga, aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari. Alisema uhakiki huo utaanza rasmi Oktoba mwaka huu ambapo vyama visivyo na sifa ya kuendelea kuwa katika Daftari la Msajili vya Vyama vya Kijamii, vitafutwa kabisa. Akizungumzia sababu zinazoweza kusababisha vyama hivyo kufutwa katika daftari hilo, alisema ni pamoja na kutolipa ada za mwaka kwa wakati na kutowasilisha kwa Msajili taarifa za kila mwaka za utendaji kazi wa chama. Sababu nyingine ni chama kufanya shughuli tofauti na zile ambazo ziliandikishwa kwenye katiba ya chama husika. "Ili kuvishirikisha vyama husika, kabla ya kuanza uhakiki huu Wizara itachapisha katika baadhi ya magazeti majina ya vyama vyote vya kijamii vilivyopo katika kumbukumbu za daftari hilo. "Baa

TANZANIA YASHAURIWA KUWEKEZA KATIKA MAENDELEO YA WATU WAKE

T ANZANIA inatakiwa kuwekeza zaidi katika watu wake ili kuweza kufikia maendeleo ya kweli na endelevu. Imesemekana, kuwekeza katika watu kumethibitisha kuwa moja ya sababu kubwa ya kufikia maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya mataifa mbalimbali na pia kuwa kati ya mambo muhimu yanayozingatiwa na wawekezaji wanapochagua maeneo ya kuwekeza. Kauli hiyo ni kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Jamii na Uchumi (ESRF), Dkt. Hoseana Lunogelo, alipokuwa akiongea wakati wa mkutano watatu wa kitaifa wa taasisi hiyo hivi karibuni jijini Dar es Salaam. "Kwa kuwekeza katika watu, Serikali itahakikisha kuwa wananchi wanawezeshwa kuendesha maisha na kuwa wenye mchango kwa jamii," alisema Dkt.Lunogelo. Alisema kuwa kuwepo kwa nguvukazi kubwa yenye ujuzi ni faida kwa wawekezaji wa ndani na nje. Alisema kuwezeshwa huko kunaleta ujuzi, maarifa na ufanisi ambao huimarisha ubora wa nguvukazi. "Nguvukazi yenye ujuzi ni muhimu sana katika kuhakikisha kuwa rasi

Mwanafunzi wa Darasa la tatu abakwa,

Mwanafunzi wa Darasa la tatu abakwa, Mwanafunzi wa Darasa la tatu katika shule ya Msingi Busunzu B Wilayani Kibondo amelazwa katika hospitali ya Wilaya  hiyo  baada ya kubakwa  na kijana mmoja alietajwa kwa jina la Lukelegwa Maneno Mkazi wa Kijiji cha Busunzu B. Akizungumza na na waandishi wa habari , Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma Dr. Adam Jonathani amesema mtoto huyo wa Kike mwenye umri wa Miaka 10, amepata majeraha makubwa  na inaonyesha amechomwa na kitu chenye ncha kali sehemu zake za sili baada ya kubakwa. Dr. Jonathani amesema mtoto huyo hali yake inaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu hospitalini hapo na kwamba kwa sasa wanaendelea kumtibu  Ugonjwa wa Maralia uliongundulika katika hatua za uchunguzi wa awali. Hata hivyo Dactari huyo hakuwa tayari kuzungumza  kwa uwazi juu ya hali halisi ilivyo kulingana na uchunguzi ulifanywa na waganga wa hospitali hiyo juu ya huyo mtoto. Aidha  jeshi la polisi Wilayani Kibondo

Ukawa wasumbua vichwa vya Baadhi ya Wabunge Dodoma

Picha
KATIKA hali inayoonekana kama kutaabishwa na wajumbe wa kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mwenyekiti wa Bunge la Katiba Swmweli Sita Samuel Sitta, jana aliamua kueleza hali halisi ilivyo kwa takribani dakika sita akiwa ndani ya ukumbi wa Bunge wakati mjadala wa katiba ukiendelea  na kuwaita  wajumbe kuwa  ni waigizaji. Hatua hiyo ya Sitta, ilibadili upepo wa Bunge kwa muda, kwani baadhi ya wachangiaji wa mjadala wa sura za rasimu ya katiba, nao waliamua kuanza kujadili hoja na kujikita kuwataka wana  UKAWA kuwa wakeli. Miongoni mwa wajumbe waliochepuka kwenye mjadala na kuwajadili UKAWA ni Mwenyekiti wa UPDP, Fahami Dovutwa, ambaye alizungumzia kuhusu makubaliano ya kikao baina ya vyama vinavyounda Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), na Rais Jakaya Kikwete. Licha ya kuwafurahisha wajumbe wa CCM, Dovutwa alijikuta akitofautiana na Mwenyekiti wa TCD, John Cheyo (UDP), pale alipokiri kwamba yeye, Cheyo na Augustine Mrema (TLP

SWALA kuanza utafiti upatikanaji nishati

KAMPUNI ya Mafuta na Gesi ya Swala (Tanzania), imetangaza rasmi kuanza kwa mpango wake wa mwaka 2014 kuanza utafiti wa upatikanaji wa nishati ujulikanao kama 2D. Lengo la utafiti huo ni kusaidia kupata taarifa za nishati zitokanazo na tetemeko la ardhi kwenye bonde la Moshi, mpango ambao upo ndani ya leseni ya utafutaji nishati Pangani Kaskazini mwa Tanzania. Akizungumzia kuanza kwa utafiti huo mwanzoni mwa wiki hii, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, David Rigde, alisema utafiti huo wa nishati itokanayo na matetemeko ya ardhi, unafanywa kama mwendelezo wa mpango uliyowahi kufanikiwa kwa kiasi kikubwa ndani ya maeneo hayo yenye leseni mwaka 2013, ambayo matokeo yalionyesha kwamba angalau bonde moja lina mrundikano wa mchanga wenye unene wa mita 3,000,430. Aidha, utafiti huo wa nishati itokanayo na matetemeko ya ardhi unafanywa kama mwendelezo wa mpango uliowahi kufanikiwa kwa kiasi kikubwa ndani  ya  maeneo hayo yenye leseni  ya mwaka 2013 ambapo matokeo  yalionyesha kwamba an

Mahakamani kwa kuendesha gari kizembe na kusababisha vifo

Mkazi wa mwanza aliyekuwa anaendesha basi lililopinduka na kuuwa watu wawili wilayani kakonko mwanzoni mwa wiki iliyopita amefikishwa katika mahakama ya wilaya ya kibondo na kufunguliwa kesi ya usalama bara barani namba 19 ya mwaka 2014 kisha kushitakiwa kwa makosa saba likiwemo la kusababisha vifo kwa uendeshaji wa gari  kizembe Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya kibondo bw Esmael Ngaile mwendesha mashitaka wa polisi bw Frank Ruvanda amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa nib w Kalim Suleiman kwa jina maarufu msangi  mwenye umri wa miaka 40 mkazi wa jijini mwanza Bw Ruvanda amesema kuwa mnamo Septemba 08 mwaka huu majira ya saa tano na nusu asubuhi katika bara bara ya kakonko nyakanazi eneo la kanyonza mtuhumiwa alikuwa akiendesha gari lenye namba za usajiri T 273 ACX aina ya Scania bus kutoka kigoma kwenda kahama  na aliendesha gari hilo kwenye bara bara ya umma kwa uzembe na kushindwa kulimudu na hatimae kupinduka Aidha bw Ruvanda amesema kuwa mtuhumiwa ameshitakiwa k

Aua Mwanafunzi ala Ubongo, Aijikata sehemu za siri

Picha
FRANCIS Fortunatus (9), mwanafunzi wa darasa la tatu Shule ya Marangu Hills Academy, ameuawa kinyama na mtu anayedaiwa kuwa mfanyakazi wao baada ya kumcharanga kwa mapanga kichwani na kisha kula ubongo wake. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Robert Boaz, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo. Alisema mwanafunzi huyo alifariki dunia juzi majira ya saa 1:20 asubuhi nje ya lango la kuingilia nyumbani kwao, Kijiji cha Samanga, Kata ya Marangu Mashariki. Kamanda Boaz, alisema muuaji ametambuliwa kuwa ni Lawrence Mramba (22), ambaye inadaiwa alishikwa na mapepo yaliyosababisha pia kukata uume wake na kuanza kuutafuna kabla ya kupoteza maisha baada ya kufikishwa Hospitali ya Kilema, Moshi Vijijini. “Polisi tunaendelea na uchunguzi wa kina wa kifo hicho, lakini mtuhumiwa wa mauaji hayo, baada ya kumuua mwanafunzi huyo aliamua pia kujikata kwa panga sehemu zake za siri. Miili ya marehemu hao imehifadhiwa Hospitali ya Kile

Wagundua mchezo mchafu

Picha
Viongozi wa Cma cha Demokrasia na maendeleo WAKATI Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ikiendelea na kikao chake jijini Dar es Salaam, Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe, amekacha. Zitto ambaye katika siku za hivi karibuni aliibua mjadala kwenye vyombo vya habari, hasa alipoingia kwenye malumbano na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, amekacha kikao hicho na badala yake ametoa taarifa ya kusafiri nje ya nchi. Kwa mujibu wa habari hizo, taarifa iliyotolewa kwa wajumbe wa mkutano huo na Mwenyekiti wa CHADEMA taifa, Freeman Mbowe, ilisema kuwa Zitto yuko safarini nchini Sudan, lakini anatarajia kuhudhuria mkutano huo wakati wowote. Habari kutoka ndani ya kikao hicho kinachofanyika kwenye Hoteli ya Blue Pearl, jijini Dar es Salaam zilieleza kuwa baadhi ya wajumbe wameonyesha dhahiri kukerwa na hatua ya naibu katibu mkuu huyo kutoshiriki. Waliolalamikia hatua hiyo walisema kuwa limekuwa jambo la kawaida kwa Zitto kutohudhuria vikao muhimu vya cham

Serikali yatakiwa kuandaa utaratibu wa ajira kwa wanaomaliza JKT

Picha
Majar Castory Bwegoge mkuu wa Kikosi 824 kj Kanembwa jkt Baadhi ya wahitim JKT Wahitimu JKT wakiwa kwenyeGwaride Mwemezi Muhingo   Kanembwa Kakonko Serikali imeshauriwa kuweka utaratibu wa ajira kwa Vijana wanaohitimu mafunzo ya Kijeshi katika Jeshi la kujenga Taifa JKT mara baada ya mikataba yao ya miaka miwili kuisha Hayo yamesemwa na   wahitimu wa mafunzo ya awali ya kijeshi Vijana wa kujitolea na wa Mujibu wa sheria, Oparation miaka 50 ya Muungano,   katika jeshi la kujenga Taifa, Kikosi cha 824 KJ Kanembwa JKT   kilichoko Wilaya ya kakonko Mkoa wa Kigoma, yalipokuwa yakifungwa rasmi Katika Lisara yao iliyomwa na Dora Damasi ambae ni mhitimu jkt, wamesema kuwa ni vizuri serikali kupitia jeshi hilo, kuandaa utaratibu kwa vijana wanaomaliza mafunzo yao mara baada ya mikataba kuisha ndani ya jeshi la kujenga Taifa   ili wapatiwe ajira katika Taasisi za   serikali hapa nchini kama Jeshi la ulinzi Tanzania, Takukuru Polisi na nyinginezo ili kuon

Wazazi wakataa kuchangia chakula shuleni

Picha
  Peter toyima mkuu wa wilaya ya kakonko kigoma   wananchi wa kata ya nyamtukuza wakiwa kwenye mkutano wa hadhara Mwemezi Muhingo Kakonko Baadhi ya wananchi wa kata ya Nyamtukuza wilaya ya kakonko mkoani kigoma wamaepokea kwa mawazo tofauti swala la uchangiaji wa chakula cha wanafunzi mashulenim,    baada ya mkuu wa wilaya hiyo Bw, Peter Toyima kuagiza kwenye mkutano wa hadahara kuwa nilazima watoto wote wapate chakula mashuleni. Wakazi wa kata hiyo wameiambia clouds   Tv kuwa wengi wao hawana uwezo wa kiuchumi na   wanakabiliwa na tatizo la hali ya hewa wakati wa msimu wa kilimo hali inayowafanya wapate mavuno kidogo na kushindwa kuendesha vizuri familia zao Wamedai kuwa hawawezi kuchangia chakula hicho bali ni vizuri utarati wa zamani uendelee huo huo, wa watoto kula majumbani mwao baada ya masomo Aidha wamesema kuwa nikweli mpango huo ni mzururi ila ungefanyika utaratibu wa utoaji wa chakula kwa awamu ili kuepuka kuwaumiza baadhi ya wazazi na famil

halmashauri yatakiwa kusitisha zuio la uuzaji wa mkaa kabla ya kupatikana nishati mbadala

Picha
Rojas Kosmas meneja misitu kibondo nicolaus kirunga katibu chadema wilaya ya kibondo Chama cha Demokrasia na Maendelo   CHEDEMA, wilaya Kibondo mkoani Kigoma kimeitaka Halmashauri ya wilaya hiyo kupitia Idara ya Misitu, kuondoa katazo la uuzaji wa mkaa na kuni kwa wachuuzi wadogowado kabla ya kupatikana kwa nishati mbadara ili kuepuka usumbufu katika jamii. Akiongea na Waandishi wa habari Mwenyekiti wa Chadema wilayani humo. Nichaus Kilunga, amema wakazi wengi wa kibondo mjini na vijijini, wanatumia nishati ya mkaa na kuni hivyo kuwazuia gafra bila kuwa na maandalizi ya kielimu   na tahimini za kiuchumi kwa jamii husika   ni kuleta adha kwa wanannchi wanaotegemea   mahitaji hayo kwa matumizi yao ya kila siku Asemema kuwa ni vizuri kabla ya kutumia nguvu   Idara ya misitu itoe elimu kwa wahusika, na kuhakikisha nishati mbadara inanapatikana ndipo utekelezaji ufanyike kuliko kufanya jambo kwa haraka ambalo litawagusa wengi na kusababisha malumbano yasiy