Mahakamani kwa kusababisha kifo kwa kumpa muwa unaosadikiwa kuwa na sumu

Mahakamani kwa kusababisha kifo kwa kumpa muwa unaosadikiwa kuwa na sumu

Mkazi wa kijiji cha kumsenga wilayani kibondo mkoani kigoma amefikishwa katika mahakama ya wilaya ya kibondo kwa tuhuma za mauaji ambapo inasadikika kuwa alimpa muwa wenye sumu bw Matane Ndegea na kusababisha kifo chake

Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya kibondo bw Mulokozi Kamuntu mwendesha mashitaka wa polisi bw Frank Ruvanda amemtaja mtu huyo kuwa ni Sintegeza Ally mwenye umri wa miaka 38 mkazi wa kijiji cha kumsenga

Bw Ruvanda amesema kuwa mnamo September 08 mwaka huu majira ya saa tisa alasiri bw Sintegeza ally  kwa makusudi alimuua  bw Matane Ndegea kwa kumpa muwa wenye sumu ambao ulipelekea kifo chake

Hakimu mkazi bw Kamuntu ameahilisha kesi hiyo mpaka itakapotajwa tena September 30 mwaka huu na mshitakiwa hakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauji hivyo mshitakiwa yuko rumande kutokana na kwamba kesi yake haina mdhamana

 Mwisho 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao