Wazazi wakataa kuchangia chakula shuleni



 
Peter toyima mkuu wa wilaya ya kakonko kigoma
 
wananchi wa kata ya nyamtukuza wakiwa kwenye mkutano wa hadhara
Mwemezi Muhingo Kakonko

Baadhi ya wananchi wa kata ya Nyamtukuza wilaya ya kakonko mkoani kigoma wamaepokea kwa mawazo tofauti swala la uchangiaji wa chakula cha wanafunzi mashulenim,   baada ya mkuu wa wilaya hiyo Bw, Peter Toyima kuagiza kwenye mkutano wa hadahara kuwa nilazima watoto wote wapate chakula mashuleni.

Wakazi wa kata hiyo wameiambia clouds  Tv kuwa wengi wao hawana uwezo wa kiuchumi na  wanakabiliwa na tatizo la hali ya hewa wakati wa msimu wa kilimo hali inayowafanya wapate mavuno kidogo na kushindwa kuendesha vizuri familia zao


Wamedai kuwa hawawezi kuchangia chakula hicho bali ni vizuri utarati wa zamani uendelee huo huo, wa watoto kula majumbani mwao baada ya masomo

Aidha wamesema kuwa nikweli mpango huo ni mzururi ila ungefanyika utaratibu wa utoaji wa chakula kwa awamu ili kuepuka kuwaumiza baadhi ya wazazi na familia zao kwakuwa wengine kipato chao ni kidogo

Mkuu huyo wa wilaya ya kakonko amesema kuwa kuna mambo mengi yanayochangia kushuka kwa kiwango cha elimu katika shule za msingi na sekondari ikiwemo wanafunzi kutokupata chakula cha mchana mashuleni hali inayowafanya watoto kutokufatilia masomo ipasavyo

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao