Mahakamani kwa kujifanya Afisa wa usalama wa Taifa

Mahakamani kwa kujifanya Afisa wa usalama wa Taifa

Mkazi wa Kinyerezi jijini Dar es salaam amehukumiwa kifungo cha miezi 24 jela au faini ya shilingi laki moja na nusu katika mahakama ya wilaya ya kibondo mkoa wa kigoma, baada ya kukili makaosa ya kujifanya mtumishi wa serikali wa jeshi la wananchi Tanzania na kujifanya afisa usalama wa taifa  

Mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya kibondo bw Erick Marley mwendesha mashitaka wa polisi bw Frank Ruvanda amemtaja mtu huyo kuwa ni Wiston Ezekiel Bulinjie mwenye umri wa miaka 38 mkazi wa kinyerezi dar es salaam

Bw Ruvanda amesema kuwa mnamo Agost 12 mwaka huu majira ya saa 9 alasiri bw Bulinjie alikwenda kikosi cha 824 KJ kanembwa Jkt wilayani kakonko alijitambulisha kwa Erast Sebasitian Tesha kuwa yeye ni askari wa jeshi la wananchi Tanzania kitu ambacho hakikuwa cha kweli , tarehe hiyo hiyo majira ya saa11 jioni akiwa kibondo mjini alijitambulisha kwa Godifrey Mpigwa kuwa yeye ni afisa usalama wa taifa

Kesi hiyo ilikuwa inakuja kwa ajiri ya kutajwa ndipo mshitakiwa akaomba akumbushwe makosa yake na baada ya kukumbushwa alikili kutenda makosa hayo kisha hakimu mfawidhi Erick Marley akamuhukumu kifungo cha miezi 24 au kulipa faini ya shilingi laki moja na nusu kwa makosa yote mawili hata hivyo mtuhumiwa amelipa faini hiyo  na kuachiliwa huru

Mwisho 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao