halmashauri yatakiwa kusitisha zuio la uuzaji wa mkaa kabla ya kupatikana nishati mbadala


Rojas Kosmas meneja misitu kibondo



nicolaus kirunga katibu chadema wilaya ya kibondo

Chama cha Demokrasia na Maendelo  CHEDEMA, wilaya Kibondo mkoani Kigoma kimeitaka Halmashauri ya wilaya hiyo kupitia Idara ya Misitu, kuondoa katazo la uuzaji wa mkaa na kuni kwa wachuuzi wadogowado kabla ya kupatikana kwa nishati mbadara ili kuepuka usumbufu katika jamii.

Akiongea na Waandishi wa habari Mwenyekiti wa Chadema wilayani humo. Nichaus Kilunga, amema wakazi wengi wa kibondo mjini na vijijini, wanatumia nishati ya mkaa na kuni hivyo kuwazuia gafra bila kuwa na maandalizi ya kielimu  na tahimini za kiuchumi kwa jamii husika  ni kuleta adha kwa wanannchi wanaotegemea  mahitaji hayo kwa matumizi yao ya kila siku


Asemema kuwa ni vizuri kabla ya kutumia nguvu  Idara ya misitu itoe elimu kwa wahusika, na kuhakikisha nishati mbadara inanapatikana ndipo utekelezaji ufanyike kuliko kufanya jambo kwa haraka ambalo litawagusa wengi na kusababisha malumbano yasiyokuwa  na ulazima.


Aidha amesema sasa uongozi wa Halmashauri kupitia Idara ya misiti wilayani humo iondoe zuio hilo, kasha  ikae na wauzaji na watumiaji wa mazao hayo ya misitu ili elimu itolewe juu ya utunzaji wa mazingira na tozo zote za mazao ya misitu na watu wote waweze kelewa ni jlipi la kufanya

Kwa upande wake Katibu wa Chama hicho wilayani humo, amedai kuwa kwa kuendeleza zuio hilo, bila utaratibu maalumu ni kukiuka haki za Binadamu kwa kuwa hali hiyo inawanyima watu mahitaji yao ya lazima

Nao wafanyabiashara ya mkaa wamesema kuwa hatua hiyo iliyotangazwa tarehe 13/ agust 2014 kuwa ifikapo  agust 18 /2014 hakuna mtu yeyote atakayeruhusiwa kutembeza mkaa mitaani kwa ajili ya biashara bali kila mtu akatafute kibali, imewafanya waishi kwa kuhangaika kwa sababu tangazo hilo limetoa muda mfupi sana kwakuwa  garama za kupata vibali hivyo shilingi laki 2 na 60 ni kubwa kulingana na kipato chao


Watumiaji wa bidhaa hiyo ambayo inaonekana  kuwa adimu kabisa  siku hizi, na kuuzwa kwa bei kubwa  ya shilingi 50,000 kila gunia,  tena usiku wa manane wanaeleza adha ambazo wanakumbana nazo kwa sasa kutokana na watu ambao wamekuwa wakiiuza kwa kutembeza katika mitaa mbalimbali mjini kibondo.



Kwa upande wake meneja Misitu  wa wilaya hiyo Rojas simony alipoulzwa kuhusu swala hilo amesema kuwa nikweli jambo hilo lipo ila watu walitaarifiwa mapema juu ya utaratibu unaotakiwa kwa wafanyabiashara wa mazao ya misitu kulingana  na sheria na nataratibu

Hata hivyo amedai kuwa  wauza mkaa na watumiaji watahathirika ila yeye hawezi kuacha sheria inavunjwa huku akiwa anaona, pamoja hali kuwa ngumu kwa walengwa na hakuna aliyezuiliwa kufanyabiashara bali kinachotakiwa ni kufuata sheria zilizowekwa

Nishati hiyo ya mkaa na kuni imeonekana imeanza kuuzwa kwa magendo mjini humo, tena kwa bei kubwa hali ambayo imelalalamikiwa na baadhi ya wuzaji na watumiaji, kabla ya zuio, gunia moja la mkaa lilikuwa linauzwa shilingi 15000/ ila hivi sasa linauzwa kiasi cha shilingi 50,000/ garama ambayo imeonekana kuwa kubwa zaidi

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao