Mwanafunzi wa Darasa la tatu abakwa,

Mwanafunzi wa Darasa la tatu abakwa,

Mwanafunzi wa Darasa la tatu katika shule ya Msingi Busunzu B Wilayani Kibondo amelazwa katika hospitali ya Wilaya  hiyo  baada ya kubakwa  na kijana mmoja alietajwa kwa jina la Lukelegwa Maneno Mkazi wa Kijiji cha Busunzu B.

Akizungumza na na waandishi wa habari , Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma Dr. Adam Jonathani amesema mtoto huyo wa Kike mwenye umri wa Miaka 10, amepata majeraha makubwa  na inaonyesha amechomwa na kitu chenye ncha kali sehemu zake za sili baada ya kubakwa.

Dr. Jonathani amesema mtoto huyo hali yake inaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu hospitalini hapo na kwamba kwa sasa wanaendelea kumtibu  Ugonjwa wa Maralia uliongundulika katika hatua za uchunguzi wa awali.

Hata hivyo Dactari huyo hakuwa tayari kuzungumza  kwa uwazi juu ya hali halisi ilivyo kulingana na uchunguzi ulifanywa na waganga wa hospitali hiyo juu ya huyo mtoto.

Aidha  jeshi la polisi Wilayani Kibondo limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba juhudi za kumfikisha mahakamani mtuhumiwa aliyehusika katika tukio hilo zinaendelea baada ya kukamilisha ushahidi.
Mwisho



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao