ILEMELA KUENDELEA KUIMARISHA MTANDAO WA BARABARA

 

Moja ya eneo la Barabara zinazojengwa na Tarura Kiwango cha Lami Kagua Nyamhongo Mwanza

Stephan Malimi 

Bahati Ezekiel Mwananchi

Sobe Makonyo Meneja wa Tarura Wilaya ya Ilemela


Ujenzi wa Barabara  za Busweru Busenga km 3 na Buswelu Kagua hadi Barabara kuu ya Mwanza Musoma kilomita 9 ni moja ya hatua ambazo zimesaidia kuondoa changamoto ya mawasiliano ya maeneo tofauti  na kurahisha usafiri kwa Wananchi Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza

Baadhi ya Wakazi Wakagua, wameeleza kuwa awali wamekuwa wakipata shida kubwa ya kusafirisha wagonjwa kwenda hospitali wakati mwingine vilitokea vifo kwa watumiaji wa vyombo vya Moto kutokana na ubovu wa Barabara

Wananchi haoStephan Malimi na Bahati Ezekiel  wameeleza kwa kuipongeza serikali hatua hiyo ya ujenzi wa Barabara kilomita 9 kwa kiwango cha Lami, kwani kwa sasa yapo mawasiliano ya karibu na haraka na maeneo ya Nyamadoke na Nyamhongolo Barabara kuu ya Mwanza Musoma, japo ni eneo dogo lakini siku za nyuma walipata adha kubwa

‘’Tunashukuru kwa hili jambo maana kutoka hapa hadi Igoma tulikuwa tunatozwa shilingi 4000 mpaka tano lakini baada ya kukamilika Barabara, tunatozwa shilingi 1500 hadi 2000 na kwa kuwa tumewekewa ata taa za Barabarani hatuna shida hata usiku tunatembea bila wasiwasi’’amesema Malimi’’

Hata hivyo lai imetolewa kwa wananchi hao kuhakikisha miundombinu hiyo inatunzwa ili iweze kutumika kwa muda mrefu ameeleza Meneja wa  Tarura Wilaya ya Ilemela Sobe Makonyo

Aidha Mhandisi Makonyo  ameongeza kuwa Barabara hizi zinakadiliwa zitumike kwa muda wa miaka 20  na si kwamba muda huo ziwe zimeharibika kabisa ila tu zinaweza kuwa zinafanyiwa ukarabati mdogo, zinahitajika kutumika kwa muda mrefu huku akiwataka Wananchi kuwa watunzaji wa miundombinu hiyo

Wilaya ya Ilemela ina Mtandao wa Barabara za aina tofauti zipatazo  kilomita 875 ambapo zimo za Zege, Mawe na Vumbi, huku mtandao wa lami ukiwa ni kilomita 50 na Barabara  hizo mpya, zenye urefu wa kilomita 12 hadi kukamilika kwake zinagarimu kiasi cha 23 bilion

 

 

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HALMASHAURI YA KIBONDO KULIGAWA JIMBO LA MUHAMBWE

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

40 CHADEMA KIBONDO WAJIONDOA