Wadau wa Elimu kusaidia vifaa kwa Wanafunzi kuongeza chachu ya ujifunzaji
![]() |
Ukosefu wa vifaa muhimu vya shule kama vile
madaftari na kalamu umetajwa kuathiri pakubwa maendeleo ya wanafunzi wa shule
za msingi katika Kata ya Kibirizi Manispaa ya Kigoma Ujiji na kupelekea wengi
kushindwa kuendelea na masomo.
Hayo yameelezwa na Afisa Elimu Kata ya Kibirizi
Manispaa ya Kigoma Ujiji Gaston Mwanache, wakati wa hafla ya kutoa zawadi ya
vifaa vya shule kwa wanafunzi wa shule za msingi Bushabani na Kibirizi
waliofanya vizuri katika masomo yao mwaka uliopita 2025.
Amesema ukosefu wa vifaa vya shule kwa wanafunzi wa
shule za msingi katika kata hiyo ni changamoto kubwa inayotokana na hali duni
za baadhi ya familia na baadhi ya wazazi kutowajibika ipasavyo katika malezi ya
watoto wao kwa kuwaacha wakilelewa na bibi zao.
Kwa upande mwingine badhi ya walimu wa shule za msingi Bushabani na
Kibirizi wamewapongeza wadau wa elimu wakiwemo Taasisi ya Kigoma Elimu
Foundation kwa kutoa zawadi kwa wanafunzi wanaofanya vizuri katika masomo yao,
wakieleza hatua hiyo imeongeza hamasa kwa wanafunzi kusoma kwa bidii.
Walimu hao Mikidad Majojo na Yasin Bubelwa wameeleza
kuwa Mwanafunzi anapokosa Mahitaji anakosa ujasili katika kujituma kufanya kazi
za darasani hivyo hawa Wadau wamekuwa wakisaidia kuongeza nguvu pale wazazi
wanapokuwa wameishia na pia uleta changamoto kwa wanafunzi kuongeza bidii ya
ujifunzaji.
Taasisi ya Kigoma Elimu Foundation imeanza programu ya
kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za msingi kumi na mbili katika Manispaa ya
Kigoma Ujiji miaka saba iliyopita ambapo mkurugenzi wa taasisi hiyo Anzuruni
Kiroboto, amesema program hiyo imeleta mabadiliko chanya.






Maoni
Chapisha Maoni