Shukran kwa wanaosaidia katika Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
Viongozi wa Dini ya Kiislam mkoani Kigoma wamepongeza
taasisi na watu binafsi wanaojitokeza na kutoa sadaka ya Iftar kwa waislam
waliofunga kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Hayo yamejiri wakati Taasisi ya The Islamic Foundation
ilipotoa sadaka ya Futari pamoja na chakula cha daku, kwa waislam waliofunga
katika Manispaa ya Kigoma Ujiji kama sehemu ya kuimarisha funga zao.
Viongozi hao wakiwemo Macho Hamisi Feruz, Sheikh wa
Kata ya Gungu katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Sheikh Bazir Ismail, Naibu
Amir Mkoa wa Kigoma Jamaat Answer Suna, wamesema hatua hiyo inawatia nguvu
waislam kuendelea na funga yao kwa furaha na usalama.
Baadhi ya waislam waliopokea zawadi hizo ambazo
zinajumuisha mchele, sukari, mafuta na tende, wameishukuru Taasisi ya The
Islamic Foundation, na kuiombea izidi kudumu ili iweze kugusa maisha ya watu
wengi zaidi katika shughuli zake za kuhudumia jamii.






Maoni
Chapisha Maoni