Watendaji ongezeni jitiada elimu na hamasa masuala ya Lishe
![]() |
| Tumain Munna Afisa Lishe Wilaya ya Kibondo |
![]() |
| Halima Madenge Mshiriki |
Mkuu wa wilaya ya Kibondo kanali Mstaafu agrey magwaza amewataka
watendaji wa kata kuhakikisha wanasimamia zoezi la wazazi kuchangia chakula
mashuleni Hali ambayo itaongeza hamasa ya watoto kuelewa kile wanachojifunza na
kuwafanya kuwa na afya bora
Ameyasema hayo wakati wa kujadili taarifa ya Hali ya lishe Kwa
watoto katika kipindi Cha robo ya tatu ya October hadi December ambapo amesema
Kila mzazi anatakiwa aone umuhimu wa kuchangia chakula kwaajili ya watoto ili
waweze kufikia malengo yaliyokusudiwa
Aidha agrey amewataka walimu kutumia maeneo ya yaliyo wazi
kwaajili ya kilimo na kuzalisha chakula ambacho kitasaidia kuendelea kuboresha
afya za wanafunzi Hali ambayo itasaisaidia pia kupunguza wingi wa michango ya
chakula Kutoka Kwa wazazi
Fundi Hamisi Mtendaji Kata ya Kitahana na Marushwa Marushwa Mtendaji
Kata ya Lugongwe wameahidi kuendelea kufanya utekelezaji hasa katika
kuhamasisha na kuelimisha jamii kutambua umuhimu wa Lishe kwa Watoto na kujitoa
kuchangia chakula mashuleni
‘’Japo uelewa bado ni mdogo katika jamii zetu, hali ambayo imekuwa
ikipelekea wengi kuchajali, ila
tunaendelea kuwaelimisha wananchi , na hali itakuwa nzuri tu kuelekea malengo
mahususi’’ amesema Hamisi
Kwa wake upande afisa lishe wilaya ya Kibondo Tumaini Muna amesema Hali
ya lishe inaendelea kuimalika huku akiwaomba viongizi wa vijiji na kata
kuendelea kutoa elimu Kwa wazazi kuhusu utoaji wa vyakula vyenye lishe ili
kuimarisha afya ya motto





Maoni
Chapisha Maoni