Mabadiliko ya Ongezekola Idadi kubwa ya Wanafunzi 2027, Mikakati iongezeke ujenzi wa Miundo mbinu

 





Mwanza. Kutokana na mabadiliko ya Mitaala ya Elimu katika shule za Msingi na Sekondari hapa nchini, hatua itakayopelekea Wanafunzi wengi kumaliza elimu ya Msingi kuelekea sekondari, serikali imeshauliwa kulitazamaa kwa jicho la pekee suala la ujenzi na uanzishwaji wa shule za sekondari ili kuleta tija

Darasa la saba na sita ni makundi yanayotarajiwa kumaliza elimu hiyo huku idadi ya shule na vyumba vya madarasa vikiwa ni vichache hatua inayotajwa kuwa huenda ikakwamisha malengo mahususi

Hayo yameelezwa na  Madiwani wa Halmashauri ya Magu Mkoani mwanza walipokuwa wakijadili Bajeti ya Halmashauri hiyo ya 2026/27ambapo  John Ngagaje Diwani Kata ya Shisha  na Jackson  LugwishaKata ya Lutale wanasema  kuwa ni vema pia bajeti hiyo ikajielekeza kunusulu sekta ya elimu  hasa kwenye miundombinu

Awali akisoma taarifa ya rasmu ya Bajeti hiyo Afisa Mipango wa Halmashauri ya Magu Mofeni Mwakajonga amesema Bajeti hiyo imetia hatua zote za kisheria na imezingatia Mahitaji yote huku  Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Edwad Kihamba akisema serikali inalitambua hilo  na akiendelea kusisitiza usimamizi mzuri wa vyanzo vya mapato  ili kufikia malengo

‘’Upo utaratiu unaendelea wa kuboresha miundombinu kwa kukarabati na kujenga kwanza shule zilizopo hivyo mpango huo uttakuwa endelevu mpata hatua malengo mahususi yatakapofikiwa’’ amesema Kihamba

Sambamba na uboreshaji wa Miundombinu ya Elimu, Watumishi wa Halmashauri pamoja na Madiwani wametakiwa kuhakikisha wanasimamia vyema Miradi na Vyanzo vya Mapato ili bajeti yenye jumla shilingi 73 bilion ilete manufaa  katika  kuwahudumia wanancnhi anaeleza Diana Philemon Makamu Mwenyeki Halmashauri ya Magu

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HALMASHAURI YA KIBONDO KULIGAWA JIMBO LA MUHAMBWE

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

40 CHADEMA KIBONDO WAJIONDOA