Mkoani Kigoma,Serikali ya Wadau kuendelea kuboresha huduma zaAfya

 

Serikali kwa kushirikiana na wadau wameendelea kupiga hatua muhimu kuelekea kufikia malengo endelevu ya mwaka 2030 ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kufikia vifo 70 kwa vizazi hai laki moja na vifo vya watoto wachanga kufikia vifo 12 katika vizazi hai elfu moja.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro, aliyewakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Dkt. Rashid Chuachua kwenye uzinduzi wa mradi wa Mjamzito na Mtoto Salama utakaotekelezwa na Shirika la Thamini Uhai, ukilenga kuchangia katika juhudi za serikali za kupunguza vifo vya uzazi na watoto wachanga.

Amesema hatua hizo ni pamoja na kuboresha na kuimarisha miundombinu pamoja na vifaa tiba kwenye sekta ya afya, na kwamba juhudi zinazofanywa na wadau kama vile Shirika la Thamini Uhai ni muhimu katika kufikia malengo hayo.
















Mwakilishi kutoka Wizara ya Afya Joachim Masunga, amesema kupitia mradi wa Mjamzito na Mtoto Salama, utaleta tija kubwa kwenye jitihada za kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Thamini Uhai Banzi Msumi, amesema mradi wa Mjamzito na Mtoto Salama ni wa miaka mitano na utatekelezwa katika mikoa mitatu ya Kigoma, Geita na Katavi, unakwenda kuimarisha maeneo muhimu manne ya huduma jumuishi za Mama na Mtoto.


 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Shule ya msingi Nengo ya Walemavu, iliyoko wilayani Kibondo mkoani kigoma, inayohudumia wanafunzi walemavu wa mahitaji maalum inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni ukosefu wa maji Vifaa vya kujinfunza na kufundishia na vyombo vya kulia chakula