2,352 Walioacha Masomo Mkoani Kigoma kureshwa Mashuleni

 












Farida Sebalua Afisa Elimu UNICEF Kigoma

Simon Siro Mkuu wa Kigoma


Kigoma
. Mkoa wa Kigoma kupitia mradi wa Elimisha Mtoto umefanikiwa kuwarejesha shuleni watoto 2,352 waliokuwa wameacha shule kupitia mfumo rasmi au nje ya mfumo rasmi.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro, kwenye kikao cha kuendeleza kampeni ya kuhimiza uandikishaji na kuwarejesha watoto walio nje ya shule iliyozinduliwa Desemba  mwaka 2025.

Balozi Sirro, amesema kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2026 bado wapo watoto wenye umri wa kati ya miaka 6 na 15 ambao hawajaandikishwa shuleni katika mfumo rasmi au nje ya mfumo rasmi wa shule na kwamba serikali kwa ushirikiano na Shirika la Kuhudumia Watoto Duniani UNICEF na wadau wengine inalenga kuwandikisha watoto wote ambao hawajaandikishwa na kuwarejesha walioacha masomo kutokana na sababu mbali mbali.

Kwa upande wake Afisa Elimu kutoka UNICEF, Ofisi ya Kigoma Farida Sebalua, amesema tafiti zinaonyesha kuwa mkoa wa Kigoma unakabiliwa na tatizo la mdondoko huku akibainisha sababu za tatizo hilo.

Mradi wa Elimisha Mtoto unaofadhiliwa na Education Above All, ukishirikiana na UNICEF pamoja na serikali ulianza kutekelezwa mwaka 2022 na utahitimishwa mwaka 2027, ukichangia juu ya kile ambacho serikali ilikianzisha kwenye program ya MEMKWA.

 

 

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HALMASHAURI YA KIBONDO KULIGAWA JIMBO LA MUHAMBWE

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

40 CHADEMA KIBONDO WAJIONDOA