Machapisho

Jamii wilayani Kibondo imetakiwa kufuata taratibu za usafi kwa kutokuuza na kula, kiholela vyakula kama mbogamboga na matunda yaliyomenywa ili kuepuka magonjwa ya mlipuko yatokanayo na uchafu

Picha
Mwemezi Muhingo Kibondo Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma Bi. Ruth Msafiri, amepiga marufuku watumishi wa serikali Wilayani humo kuacha kufanya kazi kwa mazoea jambo ambalo amesema linaweza kukwamisha ufanisi katika shughuli za umma Wilayani Kibondo. Bi. Msafiri aliyasema hayo jana katika kikao kilichowahusisha   watumishi wa idara ya afya wilayani kibondo, wakiwemo viongozi kutoka taasisi mbalimbali wilayani humo, lengo ikiwa ni kujadili namna ya kuweka tahadhari ili kukabiliana na ugonjwa wa kipindupindu, endapo utajitokeza wilayani humo. Aidha alieleza kuwa kila mtumishi wa serikali anapaswa kuwajibika kikamilifu katika nafasi yake, ili  kuhakikisha kuwa dalili za ugonjwa huo zinakomeshwa kikamilifu, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha zoezi la usafi wa mazingira wilayani humo linafanyika kila siku za aihamisi, kwa kushirikisha watumishi wote wa serikali pamoja na wananchi. Hata hivyo amekemea vitendo vya baadhi ya watumishi wa serikali kuamua kujipa ma...

Ukakamavu ni jambo la muhimu sana katika maisha ya Binadamu kwani uujenga na kuuweka sawa mwili

Picha
Hao ni baadhi ya vijana wakiwa kwenye Gwaride la kuhitimu  katika moja ya mafunzo ya awali ya kijeshi katika kikosi cha 824 kj Kanembwa Jkt kilicho wilayani Kakonko moani Kigoma Mafunzo hayo yalifungwa rasmi na Mkuu wa mkoa wa Kigoma Bw, Issa Machibya, kwa kuwakilishwa na mkuu wa wilaya kakonko Peter Toyma na kuwapandisha kutoka daraja la clut na kuwa service Girls na Boys huku jumbe mbalimbali zikitolewa kwa ajili ya kuwaasa kufuata taratibu za nchi na kutimiza viapo vyao Vijana hao ni kwa mujibu wa sheria, hususa ni wale waliomaliza  kidato cha sita 2015 katika shule mbalimbali za sekondari hapa nchini  na kundi hilo kupewa jina la Oparation Kikwete Mkuu wa Kikosi hicho Luten Conal Amos Gerad na viongozi wengozi wengine wakiwemo maafisa wa jeshi hilo walitoa jumbe mbalimbali kwa jamii ya  kitanzania juu ya kulifahamu na kuthamini kazi zake kwani lipo kwa mujibu sheria za nchi na ni kwa ajili ya watanzania wote, huku vijana wenyewe wakitoa shukrani zao wa waza...

Ubelgiji imewashauri raia wake kuondoka Burundi, huku Muungano wa Ulaya nao ukipunguza maafisa wake wanaohudumu huko kutokana na kuongezeka kwa machafuko

Picha
Balozi wa EU nchini humo Patrick Spirlet amesema hatari ya kutokea mapigano zaidi imeongezeka. Hayo yamejiri huku idara ya Amani ya Usalama ya Muungano wa Afrika ikikutana mjini Addis Ababa kujadili mpango wa kutuma walinda amani nchini humo. Kamishna wa Amani wa AU Smail Chergui amesema atatuma maafisa nchini Uganda kuandaa mazungumzo kati ya Rais Nkurunziza na upinzani. Watu zaidi ya 200 wameuawa tangu Aprili Rais Nkurunziza alipotangaza kuwa angewania urais kwa muhula wa tatu. Alishinda uchaguzi mwezi Julai. Mnamo Alhamisi, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kauli moja lilipitisha azimio lenye mapendekezo mengi yakiwemo uwezekano wa kutumwa kwa walinda Amani, na kuwekwa kwa vikwazo. Kiongozi mmoja wa upinzani nchini Burundi tayari ameuhimiza Umoja wa Mataifa kutuma walinda usalama nchini humo. Charles Nditije, mkuu wa kundi la upinzani la UPRONA, ameambia shirika la habari la Reuters kwamba wanafurahishwa na juhudi za UN kuhimiza mashauriano lakini wamevunjwa moy...

Mamlaka ya safari za ndege nchini Urusi imepiga marufuku ndege za shirika la taifa la ndege la Misri kuhudumu Urusi, msemaji wa uwanja wa ndege Moscow amesema.

Picha
Safari za ndege kutoka Urusi hadi Misri tayari zilikuwa zimesimamishwa baada ya ndege ya Urusi kuanguka eneo la Sinai mwezi jana. Abiria wote 224 walifariki, wengi wao wakiwa raia wa Urusi. Shirika hilo la Egypt Air ndilo pekee lililokuwa limesalia likifanya safari kati ya mataifa hayo mawili. Vyombo ya habari Urusi zinasema shirika hilo limepigwa marufuku kuhakikisha linatimiza matakwa ya kiusalama. Kundi la Sinai Province, lenye ushirika na Islamic State, limedai kuhusika katika kuangusha ndege ya Metrojet nambari 9268, iliyokuwa ikitoka Sharm el-Sheikh kuelekea St Petersburg Urusi. Mataifa ya Magharibi yamesema kuna uwezekano mkubwa bomu lililipuka ndani ya ndege hiyo ikiwa angani, lakini Urusi na Misri zimesema ni mapema mno kuthibitisha hayo. Baada ya ajali hiyo, mataifa kadha, ikiwemo Uingereza, yalisitisha safari za ndege za kuingia na kutoka Sharm el-Sheikh, yakitaja wasiwasi kuhusu usalama. Ndege za Egypt Air ndizo pekee zilikuwa zinahudumu kati ya Misri na Uru...

Maafisa wa polisi nchini Tanzania wamesema kuwa wanamzuia msaidizi wa aliyekuwa waziri mkuu wa taifa hilo Edward Lowassa ili kuchunguzwa kuhusiana na uraia wake.

Picha
Kulingana na gazeti la The Citizen nchini humo,wamesema kuwa bwana Bashir Fenel Awale Ally ambaye amekuwa mtu muhimu katika kampeni za urais za bwana Lowassa atachunguzwa kuhusiana na stakhabadhi zinazotilia shaka kuhusu uraia wake. Kamanda maalum wa polisi katika eneo la Dar es Salaam, Suleiman Kova amewaambia waandishi wa habari kwamba stakhabadhi alizokamatwa nazo zinatatiza kuhusiana na taifa analotoka. Amesema kuwa wakati wa kukamatwa kwake mtu huyo alipatikana na cheti cha kuzaliwa kinachoonyesha kwamba alizaliwa tarehe 11 mwezi Julai mwaka 1969 mjini Dodoma. Kulingana na afisa huyo mshukiwa huyo pia alipatikana na pasipoti iliotoka jijini nairobi na ambayo inayoonyesha kwamba alizaliwa mjini humo mnamo tarehe 11 mwezi Julai mwaka 1969,akiwa na jina la Bashir Fenal Abdi Ally Awadhi . Mshukiwa huyo anayedaiwa kuwa mwanaharakati na mfuasi mkubwa wa chama cha upinzani Chadema alikamatwa nyumbani kwake huko Mikocheni. Kova amesema kuwa kuna ishara kwamba mshukiwa huyo ni r...

Viongozi wa Muungano wa Ulaya wanatarajiwa kutoa mabilioni ya euro kwa mataifa ya Afrika kuyawezesha kusaidia kupunguza mzozo wa wahamiaji Ulaya.

Picha
Tume ya Muungano wa Ulaya imesema itatoa €1.8bn (£1.3bn) na inatarajia mataifa zaidi ya EU yaahidi pesa zaidi. Lengo la ufadhili huo ni kusaidia kusuluhisha matatizo ya kiuchumi na kiusalama ambayo huwafanya watu kutoroka mataifa ya Afrika. Aidha, zitatumiwa kuyashawishi mataifa ya Afrika kuwapokea watu ambao wamenyimwa hifadhi Ulaya. Ahadi hiyo inatarajiwa kutolewa kwenye mkutano mkuu kuhusu wahamiaji unaofanyika Malta, na ambao ulipangwa baada ya meli iliyobeba wahamiaji kuzama Libya mwezi Aprili. Watu 800 walifariki Watu 150,000 wamevuka bahari ya Mediterranean kutoka Afrika mwaka huu, wengi wakitua Italia na Malta. Hata hivyo, mtazamo wa EU umebadilika tangu Aprili na kuangazia zaidi wakimbizi wanaotoka mashariki na hasa Syria, ambao wanawasili kwanza Ugiriki na kuvuka hadi Uturuki kisha kuelekea kaskazini kupitia bataifa ya Balkan. Zaidi ya viongozi 60 kutoka Afrika na Ulaya, akiwemo Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron, wanakutana Valletta, Malta kwa mkutano huo mkuu...

Wataalamu wa afya wanasema mpango wa chanjo kwa umma dhidi ya homa ya uti wa mgongo barani Afrika umepata mafanikio makubwa.

Picha
Zaidi ya watu milioni mbili walipata kinga dhidi ya maradhi hayo katika nchi zipatazo 16 barani Afrika, kutoka Gambia mpaka Ethiopia. Shirika la Afya Duniani limesema katika kipindi cha mwaka 2013 kulikuwa na wagonjwa wanne tu, katika bara hilo ambalo awali liliweka rekodi ya kuwa na maelfu ya vifo vinavyotokana na ugonjwa huo, kila mwaka. Kampeni ya kupambana na ugonjwa huo ilianza mwaka 2010. Kinga dhidi ya uti wa mgongo