Dc awataka Viongozi wote serikali za mitaa waliochaguliwa hivi karibuni kutimiza wajibu wao kila mmoja na kuondoa tofauti za vyama

Kibondo;  Mkuu wa wilaya ya Kibondo mkoani kigoma bw. Venance Mwamoto amewata viongozi waliochaguliwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mapema mwaka jana kufanya kazi kwa bidii katika kuchochea maendeleo ya wilaya.

Kauli hiyo aliitoa wakati akizungumza na viongozi hao katika Tarafa ya mabamba kata ya mabamba mara baada ya kuapa kulitumikia taifa na wananci kwa moyo mmoja na ushilikiano katika kudhibiti matukio machafu.

Bw.mwamoto amesema katika utawala wa serikali ngazi ya chini ni kupitia uchaguzi wa serikali za mitaa na hivyo wao wanapaswa kluwa chachu ya kuchochea maendeleo ikiwa ni pamoja  na kutoa taarifa juu ya uharifu.

Mwamoto alisema kuwa uongozi ngazi ya vitongoji ni  hatua muhimu sana kwani hakuna serikali kuu bila kuanzia ngazi ya kitongoji hivyo ni vyema viongozi hao wajiamini na kufanya kazi kwa bidii na kwa kushirikiana ili kufikia mafanikio.

Aidha aliwataka kuachana tabia ya mashindano ya kisiasa  ambayo kwa sasa hayawezi kuleta tija ila lililopo ni kushirikiana watu wa vyama vyote kwani wote wanajenga nchi moja. Kinachotakiwa ni uadilifu katika utendaji wa kazi  

Nao baadhi ya viongozi hao waliochaguliwa hivi karibuni ambao ni Samweli Jonasi na Halima Abdalah  katika uchaguzi wa serikali za mitaa wameahidi kuwatumikia wananchi waliowapa dhamana hiyo ya kuwa madarakani kwa ushilikiano bila kujali itikadi za vyama


Hata hivyo wameiomba serikali itoe mafunzo ya namna ya utendaji ka zi unao takiwa  kwa viongozi wote waliochaguliwa katika kipindi hiki ili kila mtu ajue wajibu wake kwasabau wengi wao ni wapya kwa nafasi hizo ili kuondoa mianya ya kulaumiana 
Venance Mwamoto Dc Kibondo
 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao