Madiwani Kibondo wawataka wakuu wa Idara kuwa wabunifu na waadilifu

Madiwani wa Halmashauri ya wilaya  ya Kibondo mkoani Kigoma wamewalalamikia Wataalam na wakuu wa Idara za Halmashauri hiyo kwakuonyesha uwezo mdogo au kufanya makusudi kutoibua vyanzo vya mapato  hali inayosababisha  kukosekana kwa mapato na kurudisha nyuma  maendeleo.


hayo yamebainishwa  na madiwani hao wakati wa kikao cha kujadili na kupitisha Bajeti ya fedha katika mwaka 2015/2016  kilichofanyikia mjini Kibondo wakidai kuwa vipo baadhi ya vyanzo ambavyo vipo na vinaonekana lakini katika taarifa havionekani hatua walio itaja kuwa ni kutaka kufanya ufisadi.

Diwani wa kata ya Busagara Bw Godwini Sibanilo, amemesema vipo vyanzo vingi ambavyo katika taarifa havikutajwa na huku kila siku watu wanatozwa pesa na Halmashauri hiyo ikiwa baadhi ya vyoo vilivyoko katika maeneo mengi ya mji wa kibondo

baadhi ya daiwani wakiwa kwenye kikao kwa ajili ya kujadili Bajeti ya wilwyw hiyo 2015/2016
Aidha Madiwani hao wamesema kuwa kuna miradi ambayo inajtngewa fedha zisizo kidhi mahitaji hasa kama miradi ya ujenzi kama zahanati ya kijiji cha Bitare iliengewa fedha kiasi cha sh. milon kumi na tano  hali ambayo inasababisha miradi mingi kubakia viporo kila mwaka na kuwaacha wananchi wakinung’nika kwa kutopatiwa huduma stahiki.
 
Godwini Sibanilo Diwani kata ya Busagara
Pascal Katabizi Diwani kata ya kitahana

Hadija Mauldi Diwani viti maalum kibondo mjini
Benard Andrea Diwani kata ya Misezero
Wakuu wa idara Halmasahauri wilaya ya kibondo

Insert Benard Andrea Diwani kata ya Misezero
Que in……..

Akijibu malalamiko ya madiwani hao Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya hiyo bw Judathadius Mboya , amesema sababu inayofanya baadhi ya vyanzo vingine visitajwe ni kwasababu vingine ni vidogo na kulingana na uingizaji wake kuwa mdogo inalazimika kuwatumia wale wanaokusanya mapato katika vyanzo vikubwa , kwakuwa anapoajiriwa mtu anatakiwa alipwe kima cha chini cha mshahara tsh 200,000/ wakati yeye anakusanya pesa ambazo ni kidogo.


Hata hivyo  Baraza hilo limepitisha Bajeti ya Shilingi billion 42 ambayo itajikita katika miradi ya maenedeleo katika mwaka 2015/16 katika utekelezaji wa ,miradi mbalimbali ndani ya wilaya hiyo.

 Aidha wameiomba serikali kuleta pesa mapema ambazo zinakuwa zimeombwa kupitia kwenye bajeti husika ili kutimiza malengo kwakuwa hata pesa za bajeti iliyopita wa pesa zilizofika  ni asilimia 7 tu  hali ambayo inakwamisha juhudi za kuleta maendeleo kwa wananchi .

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw, Emili Mpfanye amewataka madiwani hao kuwa waaminifu katika kusimaia miradi ya maendeleo kwa kuwatumikia wananchi wao waliowaweka madarakani  ili kuondoa malalamiko huku wakitambua kuwa huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu

Pamoja na mambo mengine baadhi ya wananchi wameukosoa utaratibu wa mchakato kutengeneza bajeti hiyo haukuzingatia ushirikiwaji wao ili nao watoe vipaumbele vyao juu ya mambo wanayoyahitaji katika maeneo yao bali ni watu wachache ambao hukaa na kupanga badala ya kuanzia kwenye vitongoji na kuja ngazi za vijiji hadi kata .


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao