Kanisa la teketezwa kwa Moto


Mabaki ya kanisa la TAG lilichomwa moto
Kanisa la teketezwa kwa Moto

Mwemezi Muhingo Kibondo


Kanisa la Tanzania Assemblies of God TAG lililoko katika kijiji cha Bunyambo wilayani kibondo mkoani kigoma limeteketea baada ya kuchomwa moto na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia  jumamosi ya wiki iliyopita tukio hilo likihusishwa na maswala ya kisiasa za kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mapema mwezi decemba mwaka jana 

Tukio hilo lilitukia usiku wa kuamkia jumapili iliyopita majira ya saa tano usiku ambapo watu wasiojulikana waliingia kanisani hapo na kupanga thamani zote za ndani ambazo zimekuwa zikitumika wakati wa ibada na kuzimwagia mafuta ya Petrol hali iliyosababisha jingo zima kushika moto

Akiongea na Clouds tv katibu wa kanisa hilo Bw Samweli Butelanya amesema kuwa tukio hilo japo hawajafahamu chanzo nini ila wao wanalihusisha na mambo ya kisiasa kwani baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa ndipo mambo hayo yametokea na kudai kuwa siku mbili kabla kanisa la Evergelist Asemblies of God Tanzania EAGT lililoko kijijini hapo watu wasiojulikana walibomoa jingo lanisa hilo na kuvunja vyombo vya muziki


Hata hivyo waumini wa kanisa hilo, ambao hawakutaka kurekodiwa waliiambia clouds kuwa swala  hilo linausishwa na mabo ya kisiasa kwa kuwa badaada ya uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika hivi karibuni Desemba mwaka jana kulianza kutokea malalamiko miongoni mwa wanakijiji kuwa kanisa hilo lilichangia kupatikana kwa ushindi wa mwenyekiti wa kijiji hicho Bw Danford Mushachi kwani hata vyombo vya muziki ndivyovilikuwavikitumika kufanya kampeni  kwani wajumbe na mwenyekiti mwenyewe wanasali katika kanisa hilo



Kufuatia tukio hilo mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama  wilaya ya kibondo bw Venance Mwamoto alifika kwenye eneo la tukio akiwa viongozi wa kamati hiyo, ili kuona hali halisi ilivyo katika kanisa hilo ambapoaliwambia waumini hao kuwa kitendo hicho sikizuri katika jamii na kuahidi kuwa mahakamani wote watakao


Aidha bw Mwamoto  aliwataka waumini wa kanisa hilo na jamii kwa ujumla kuacha tabia ya kuingiza siasa katika nyumba za ibada hali inayoweza kuleta machafuko makubwa  hapa nchini na kuwakataa na kuwatolea taarifa wale wote wanaotaka kuwagawa watanzania kwa kutumia  siasa nda yadini kwakuwa nyumba za ibada ni sehemu ya kuubiri Amani.


Nao baadhi ya viongozi Dini wilayani kibondo wameeleza kushangazwa kwao na vurugu hizo za kuchoma nyumba za ibada ni kwasababu hofu ya Mungu miongoni mwa jamii imetoweka  kama anavoeleza Dr Themeo Ndenza Askofu wa kanisa la Anglikana Dayosesi ya Kibondo


Aidha Ndenza ameitaka jamii kuwa sheria na  na taratibu za nchi haziruhusu vitendo vya aina hiyo kwani kumshinda mtu katika ushindani wa kisiasa si sa babu ya kuharibu mali za watu na kuitaka serikali kuwa macho kwani vitendo hivyo vya watu kuwa jeruhi viongozi wa dini kuwauwa na kuhabu mali vinaonekana kushika kasi huku serikali imekaa kimya hali inayoweza kuleta madhala katika jamii



Kwa upande wao baadhi ya wakazi wa kibondo ambao ni tamasha kikoti na Amani James wamekuwa na haya ya kusema juu vurugu zinazotokea na kuziusisha nyumba za ibada kuwa ni vitendo vya uvunjifu wa amani kwani Dini ni taasisi ambazo zinategemewa juu ya kuleta amani katika nchi na jamaii kwa ujumla sasa kama waumini wenyewe wameanza kuchoma maeneo ambayo ni makimbilio itakuwaje?



Hata hivyo imetajwa kuwa katika sakata la uchaguzi wa serikali za mitaa ushindani uliokuwepo ni watu wawili ambao walikuwa wagombea kupitia vyama tofauti chadema na Ccm na wote wanasali katika makanisa tofauti EAGT na TAG kijijini hapo ambapo alishinda mtu wa chadema katika nafasi ya mwenyekiti wa kijiji

Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao