Vitendo vya unyanyasaji kwa Walemavu

Vitendo vya unyanyasaji kwa Walemavu


Pamoja na jamii kupiga vita unyanyasaji walemavu bado watu wengine wanaendeleza tabia hizo ambazo ni ukikwaji wa haki za Binadamu kwa kundi hilo, baada ya mkazi mmoja wa kijiji cha Buyenzi Kata ya Itaba Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma Bw, 
Alcado Poul  kumpiga mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Alfred Jonas  ambaye  ni ulemavu na kumvunja mguu.

Tukio hilo lilitukia Desemba 31 mwaka jana  majira ya saa  kumi join wakati Bw, Alfred Jonas alipokuwa anaenda sokoni kutafutaji yake ndipo alipokutana na Bw, Alcado Poul ambaye alimshika na kumnyanyua juu kasha kumtupa chini mara mbili hali iliyo msababishia majeraa na amumivu makali hatua iliyopelekea  kulazwa katika Hospitali ya wilaya ya kibondo.

Kutokana na kuumia vibaya mguu kwa kuvunjika, mlemavu huyo amepewa rufaa kwenda Hospital ya Bugandondo jijini mwanza baada ya madaktari Wilayani kibondo kushindwa kumtibu kutokana na ukubwa wa tatizo    
Bw Alfred Jonas Akiwa amelazwa hospitalini, anaeleza mkasa kamili ulivyo mkuta hadi kujikuta anafikishwa Hospital bila kutarajia


Mwenyekiti wa chama cha watu wenye ulemavu chawata wilayani kibondo  bw.Everlisto Ngalama amewataka wananchi kuwatambua walemavu kama watu wengine na kuepuka  kutowatende vitendo vya kikatili.

Ngarama amesema kuwa.kutokana na kuwepo kwa vya unyanyasaji unyanyasaji dhidi ya walemavu hali inayo wafanya kujihihisi kama waliotengwa na jamii na kuishi kwa hofu.


Aidha Ngarama amesma kuwa Mtu huyo aspokatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria chama chake kitaitisha maandamano ya walemavu ili kudai haki zao kwakuwa mambo haya yamekuwa yakifumbiwa macho hatua inayoendelea kuchochea huku walemavu wakijihisi kuwa wao si kama Binadamu

Kwa upande wao baadhi ya wananchi ambao ni Shida Maxmilian na Jumanne Jacobo, toka kijijini hapo, wameeleza kusikitishwa kwa na kitendo alichofanyiwa mlemavu huyo na kusema kuwa ni vitendo vya kikatili na kuiomba serikali kukemea vikali watu wanao waonea wenzao bila utaratibu huku wakijua matatizo waliyonayo

Wananchi hao wameendelea kuushutumu uongozi wa kijiji hicho kwa kufumbia macho vitendo vya uharifu hali inayowatia hofu kwakuwa mtu yeyote anaweza kufanya jambo bila kuogopa lolote kama anaweza kutiwa nguni, na kudai kuwa hadi sasa mtu anaehusika kumuumiza  mlemavu huyo bado hajakamatwa

Hata hivyo, mtendaji wa kijiji cha bunyezi bw.laurenti mahwela amesema serikali ya kijiji kwa kushilikiana na wananchi wananendelea kumtafuta mhusika wa kitendo hicho ili achukuliwe hatua za kisheria.


Mwisho 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao