Wakataeni wanasiasa Mchwala


Wakataeni wanasiasa Mchwala

Mwemezi Muhingo Mwananchi

Kasulu; Watanzania wametakiwa kukataa kufuata itikadi za wanasiasa wasiokuwa na maadli na uzalendo kwa kusababisha migongano na uchonganishi katika jamii kwa ajili ya kutafuta umaalufu.

Hayo  yalisesemwa na mkuu wa wilaya ya Kasulu mkoani kigoma Dany Makanga, wakati wa kufunga mafunzo ya awali ya kijeshi, katika kikosi cha 825 kj, Mtabila Jkt kwa vijana mujibu wa sheria awamu ya pili mwishoni mwa wiki.

Makanga aliwambia mamia ya wakazi wa wilaya hiyo waliohudhulia katika mahafali hayo, kuwa kumekuwepo na tabia za baadhi ya wanasiasa wanaoeneza chuki, katika jamii ili watu walichukie kundi frani na kuwalagai kuwa matatizo yao, wao wanaweza kuwasaidia hali inayoweza kuvuluga amani.

Aidha alisema kuwa wananchi wengi wanaoishi kwenye vijiji vinavyopakana na kikosi cha jeshi cha mtabila jkt, kwa muda murefu wamekuwa wakiyumbishwa na baadhi ya watu kuwa maeneo hayo ni mali ya wanavijiji hivyo, na kudai kuwa mipika ya kikosi na vijiji haifuatwi na kuwambia kuwa wanaingiliwa kwenye mashamba yao na kuwa wananyanyaswa kwa kutolewa katika maeneo ya kendeshea shughuli za kilimo.

Eneo la Mtabila maali kilipo kikosi hicho, hapo mwanzo ilikuwa ni kambi ya wakimbizi toka nchini Burundi waliokimbia  machafuko  , na baada ya Warundi hao kurejea kwenye nchi yao, serikali ya Tanzania iliamua kubadilisha matumizi kwa kuweka jeshi eneo hilo.

Hata hivyo alisema kuwa  eneo hilo lilipokuwalinatumiwa na wakimbizi chini ya shirika la umoja wa mataifa, la kuhudumia wakimbizi mipaka ilikuwa kama ilivyo hivi sasa na watanzania ambao ni jirani waliyatumia maeneo hayo kwashughuli za kilimo na nyinginezoila ila baada ya kubadilisha matumizi, kwakuweka kikosi cha jeshi, lazima taratibu zifuatwe ili kuondoa mkanganyiko.

Aidha alidai kuwa kuwa kikosi hicho kwa hivi sasa kinaanza kuleleta wataalam wa kada mbalimbali kam kilimo Walimu,  Madakitari, pia kitakuwa na nyenzo za kufanyia kazi hivyo wananchi watanufaika na uwepo wa kikosi hicho iwapo kama watakuwa ayari kwa kushikiana na kuhitaji msahada na ushauri kutoka kwenye taasisi hiyo, 

Kikosi hicho cha Mtabila jkt, kinapakana  na vijiji vya Mugombe, Kitagata, Nyachenda, Kinazi na wannchi wa vijiji vyote hivyo walilazimika kuacha kuendesha shuguli za kilimo kwakuwa hivisasa jeshi linatumia kwa kazi zake.

Pamoja na mambo mengine wakatiwa kufunga mafunzo hayo ya kijeshi, mkuu wa mkoa wa kigoma Luten Kanal Mstaafu Issa Machibya,ambaye alikuwa mgeni rasmi, aliwataka wahitimu kuwa waadilifu na kuishi kwa kufuata maadili na taratibu za nchi kuokana na mafunzo waliyoyapata kwa kufuata kiapo walichoapa

Machibya alisema kuwa lengo la kuanzisha jeshi la kujenga Taifa ni kuwajenga vijana katika uzalendo wa kuipenda nchi yao, kuwa na nidhamu katika jamii, udugu na mshikamano, hivyo vijana wote wanatakiwa kukumbuka hayo yote kwa kuytimiza.

Vijana waliomaliza mafunzo ya kijeshi kwa mujibu sheria kikosini hapo  idadi ya ni elfu 1 miamoja1na kumi  toka vyuo mbalimbali vya ualimu na waliomaliza kidato cha sita katika shule za sekondari  ikiwa wavulana mia 7 hamsini na 5 na wasichana mia 3 hamsini na 5 Mwisho            

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao