Watu wane wa Familia moja wafariki baada ya chakula chenye sumu

Watu wane wa Familia moja wafariki baada ya chakula chenye sumu

Mwemezi Muhingo Kakonko

Watu wanne wa Familia moja wakazi wa kijiji cha Kibambila wilani Kakonko mkoa wa Kigma wamefariki dunia baada ya kula chakula kinachosadikiwa kuwa na sumu

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea jana wilayani hapo kwa kuwahusisha watu watano ambapo wanne walifariki dunia na mmoja kunurika kifo na baadae kuruhusiwa kwenda nyumbani

Mganga  aliyekuwa zamu katika kituo cha Afya cha kakonko ambacho kinatumika kama Hospitali ya wilaya  Bi, Ndalikunda Kweka, amesema kuwa watu hao walifikishwa hospitalini hapo baadhi yao   wakiwa na hali mbaya ila kadri muda ulivyokuwa ukisogea ndipo walipokuwa wakiziwa na wengine kupoteza maisha.



Nae Mganga mkuu wa wilaya hiyo Bw  Fadhili Seleman amesemakuwa kuwa mara baada ya wagonjwa hao kufikishwa hospitalini hapo walipowafanyia uchunguzi waligundua kuwa wamekula vitu vyenye sumu na baada ya kuhoji kwa waliokuwa na fahamu walisema kuwa wamekula ugali. na kuwataja majina ya waliokufa kuwa ni Neema Joseph,miaka 12 Jonas Joseph18 Yusuph Joseph na Majaliwa Joseph miaka 11 aliyefariki baadaye



Aidha Dr Fadhili ameitaka jamii kuwa ni vizuri mtu kufika haraka hosptali au kwenye kituo cha afya mara baada ya kumaliza kula chakula ili kama kuna tatizo kubwa liweze kuangaliwa kuliko kukaa kimya baadae kupata madhala makubwa kwa kuwa zipo sumu ambazo zinachukuwa muda murefu kuleta madhala katika mwili wa binadamu


Baba mzazi wa Vijana waliokufa kwa sumu Bw, Joseph Kajolo, yeye alinusurika kwakuwa hakula chakula hicho, maana alishindwa kula kwasababu ya kuwa amelewa baada ya kunywa pombe

Baadhi wananchi wa mjini kakonko waliokuwa katika kazi ya kuchimba makaburi manne kwa wakati mmoja wanaeleza maskitiko yao nakusema  vitendo hivi vimekuwa vikijirudia marakwamara watu wengi kupewa sumu hali inayowafanya kuishi kwa hofu katika jamii  


Mkuu wa wilaya hiyo, Peter Toyima amewataka wakazi wa wilaya hiyo kuachana na mambo hayo kuwadhulu watu wasiyokwa na hatia bali kila mtu anatakiwa kutambua uthamani wa Binadamu mwenzake

  
Hata hivyo mkuu huyo wawilaya amesema kuwa mtu mmoja anashikiliwa na jeshi la polisi akithumiwa kuhhusika na mauwaji hao na jeshila polisi linaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha tatizo



 
Peter Toyma Dc Kakonko
Dr Fadhili Seleman mganga mkuu Wilaya kakonko

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao