Mtoto huyu anadaiwa ameibwa, na kutelekezwa kwenye basi la Abiria na hadi sasa hajapata wazazi wake


Katika vintendo vinavyotajwa kuendelea kufanywa na wafanyakazi wa ndani kwa kuwanyanyasa vimeendele kushika kasi baada ya motto mwenye umri wa miaka mitatu hadi mine kutelekezwa kwenya basi abiria jijini Mwanza na mtu anayesadikiwa kuwa mtumishi wa nyumbani kwao.

Mtoto huyo ambaye anaweza kutaja jina lake tu la Antoni, na wala hawezi kutaja majina  halisi ya wazazi wake bali anataja mzazi wake wa kiume anaitwa Baba Antoni na mama Antoni, alikutwa amelekezwa kwenye Basi la Abiria la Kampuni ya Horeza, linalofanya safari zake kutoka Kibondo mkoani kigoma kuelekea jijini mwanza  

Wahudumu wa gari hilo walishangaa kuona abiria wote wametelemka na kumshangaa mototo huyo amebaki peke yake bila mtu mzima anaye weza kumsaidia ndipo walipojaribu kuwauliza baadhi ya abiria waliokuwa wamesalia nje ya gari gabla ya kuelekea majumbani mwao juu ya motto huyo inadaiwa mwanamume mmoja alijibu kuwa wakati wa safari alikuwa na binti mmoja anayesadikiwa kuwa na umri wa miaka kumi hivi.

Aidha wakati wa kutelemka kwenye gari walishangaa binti huyo anatoka peke yake na alipoulizwa  mbona mototo huyu una mwacha alisema kuwa yeye hamjui na kuamua kumuacha peke yake bila msahada ndipo wahudumu hao waliamua kurudisha kibondo mkoani kigoma ili kutafuta wazazi wake lakini hawakuweza kupatika na baadae kuamua kumpeleka kituo cha polisi mjini kibondo.

Kwa mujibu wa maelezo ya polisi wazazi wa motto huyo wazazi wake hawajapatikana na amechukuliwa na msamaria mwema anayeitwa Josephin Joseph ambaye ni mfanya kazi wa Jeshi la Polisi hadi hapo wazazi wake watakapopatikana kwa maana yeye hawezi kujieleza vizuri kulingana na umri wake

Hata hivyo baadhi ya wakazi wa mji wa kibondo waliokusanyika  mumtambua motto huyo,  wametoa maoni yao kuwa ni vizuri jamii ikawa makini hasa pale mtu anapohitaji mfanya kazi wa ndani kuhakikisha anafahamu kwao na wazazi wake walipo ili kuepuka madhala zaidi
Mtoto Anton anayedaiwa kuibwa na mtu anayesadikiwa ni mfanyakazi wa ndani na kutelekezwa kwenye basi la abiria

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao