Kakonko yapitisha Rasmu ya bajeti Bilion 26 mwaka 2015/16

Mwemezi Muhingo Mwananchi

Katika mwaka wa fedha wa 2015/16 Halamashauri ya wilaya kakonko Mkoani imepanga kukusanya na kutumia jula ya  Tsh Bilion 26.4kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo ruzuku ya serikali kuu bilion 25 na mapato ya ndani tsh milion 436 ambapopo mchango wa serikali kuu ni sawana asilimia 98.3 ya bajet ya Halmashauri

Akisoma taarifa yake wakatati wa kikao cha Baraza la madiwani kilifanyika mjini kakonko  kwa ajili ya kujadili mipango na Rasimu ya mapendekezo ya Bajeti ya Halmashauri hiyo, kwa mwaka wa fedha wa 2015/16  Bw, Galpa Sedoyeka, amesema kuwa vipaumbele vya bajeti hiyo nikujikita zaidi katika mswala ya elimu

Sedoyeka amesema kuwa mpango wa mwaka 2015/16  umeandaliwa kwa kuzingatia vipaumbele na kiutekelezaji  kuboresha utoaji elimu bora ili kuongeza kiwango cha ufaulu kuwaandaa wanafunzi kuweza kukabiliana na na maisha baada ya kumaliza masomo
Hata hivyo ametaja vipaumbele vingine kujenga Ofisi za Halmashauri ujenzi wa nyumba za watumishi kwa kushirikiana na Taasisi mbalimbali kama shilirika la Nyumba la Taifa [NHC] ambalo halmashauri imeingianalo mkataba wa kujenga nyumba 50

Amesema kuwa mapato ya makusanyo ya ndani yanategemea ushuru wa masoko ya mipakani mazao na leseni mbalimbali ambapo amedai kuwa wanafanya utarati kuongeza tozo ili kukabailiana hali halisi kwa kuwa halmashauri hiyo ni changa imeanzishwa mwaka 2013 na kuanza kufanya kazi mwaka 2014

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Nyamtukuza Marko Bajora, amesema kuwa bajeti hiyo inachangamoto nyingi hasa mapato ni kidogo sana hali inayoweza kumfanya mwananchi asinufaike kutokana na baeti hiyo kuwa tegemezi sana  asilimia 1.7 ndo mapato ya ndani na asilimia 93.3 inategemea kutoka serikali kuu hivyo pesa hizo zikichelewa kufika kwa muda muafaka upo uwezekano halmashauri ikashindwa kujiendesha

Bajeti hiyo kwakuwa inalenga  kumsaidia mwananchi, imepokelewa kwa mawazo tofauti na baadhi ya wananchi waliohudhulia katika kikao hicho ambapo mmojawao Bw, Mohamed Ismail ameshauri kuwa lengo la halmashari hiyo nijema ila pale inapotaka kuongeza ushuru ni vema itengeze miundo mbinu ya kukusanyia tozo hizo kwasababu katika sehemu kubwa ya wilaya hiyohakuna maeneo maaluma ya kukusanyia mapato kama machinio hali inayoweza kufanya ukusanyaji kuwa mgumu na kukosa mapato

Mkurugenzi mtendaji waHalmashauri hiyo Bi Zaina Msangi amesema kuwa pamoja na kuwa bado mambo mengi hayajakaa vizuri wanafanya mchakato wa kuboresha vyanzo vya mapato ili kuleta mafanikio katika matarajio yanayokusudiwa

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya kakonko Bw, Juma Maganga amewataka watendaji wote wa kata na vijiji,  kuweza kufanya kufanyakazi kwa bidii uaminifu katika swala la kukusanya mapato kwakuwa wakati wanawatumia mawakala ni hasara kubwa iliyopatikana

Pamoja na mambo mengine Maganga amewataka wa nanchi wa Kakonko kukubali kwenda na mabdiliko ya kimaendeleo yaliyopo kaika nchi yetu kwa kufuata taratibu na sheria

Aliyasema hayo akiwahasa wananchi kukubali kuwa nampangilio mzuri wa mji kwa kujenga na kuwa naviwanja vya makazi vilivyopimwa kwa mujibu wa sheria kufuata miongozo ya Idara ya ardhi.

Aidha alidai kuwa Mji wa kakonko hapo awali ulikuwa ni kijiji, jamii ilizoea mazingira kutegemeana na wakati uliokuwepo lakini baada ya serikali kutangaza kuwepo na wilaya na halmashauri katika eneo hilo lazima watu wakubali kufuata taratibu wanazopewa

Aliwataka kufahamu kuwa idara ya ardhi wilayani hapo, imetoa elimu kwa kiasi kikubwa kuwa kila aliyekuwa na shamba likapimwa vikapatikana viwanja zaidi ya vitatu nilazma vinavyobaki itakuwa na mali ya Halmashauri na mtu aakaye hitaji kuvimili zaidi anatakiwa kulipia kwa mujibu wa taratibu alikini cha ajabu wengi wao wamekataa kugawana viwanja na Halmashauri hiyo na kusema kuwa yeyote ambaye hatakubali kufanyahivyo, sheria itachukua nafasi yake kwa kuchukua  na wakuwamilikisha wengine kama utaratibu unavyosema na kudai kuwa agizo hilo siyo la mtu binafsi bali ni nchi nzima   
Mwisho

  

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao