Mtendaji wa kata akataliwa, wakijiji afukuzwa kazi katika mkutano wa hadhara

Mtendaji wa kata akataliwa, wakijiji afukuzwa kazi  katika mkutano wa hadhara

Wananchi wa Kijiji cha kigendeka Kata ya Busagara wilayani kibondo mkoa wa kigoma wamemmfukuza kazi Mtendaji wa kijiji, kukataa kufanyakazi na mtendaji wa Kata kwenye mkutano mkuu uliofanyika kujadili mambo mbalimbali ya maendeleo,  kwa madai kuwa wote wawili walishirikiana kugushi mhuri wa ofisi ya kijiji na kugawa ardhi hekali 100 kinyume cha taratibu

Uamuzi wa  wakazi hao umefikiwa baada kikako cha  uongozi wa kijiji hicho kilichokaa Tarehe 15.1.2015 baada ya kubaini matatizo hayo, na kumuita mtendaji huyo na kumueleza makosa yake  hali iliyowafanya wajumbe wa kikao hicho kutokuwa na Imani nae na kumtaka aachie ngazi hatua iliyofikia mwenyekiti Bw, Yotham Kitwe  kuitisha mkutano mkuu wa kijiji ili kutoa maamuzi.
 
Awali mkutanoni hapo, ilidaiwa kuwa mwaka jana tar 24.4.2014 Bw Abeli Fransisco akiwa ni mwenyekiti wa kitongoji, aliiba mhuri wa Afisa mtendaji wa kijiji  na kumgawia Bw, Samsoni Kitwe  ardhi ya kijiji hicho ambayo ilitengwa kwa kulishia mifugo  ya  jamii ya kijiji hicho na kumshirikisha Afisa mtendaji wa Kata ya Busagara Bw, Baruani Gwimo nayeye kuchukua uamuzi wa kusaini barua ya kugawa eneo hilo, Tar 27.4.2014, huku wakijua kuwa ni kinyume cha taratibu ilitengwa kwa kazi maalumu  na haikutakiwa kumilikishwa kwa mtu yeyote


  Katika hatua hiy,  uongozi wa kijiji  waliamua kusema kuwa hawako tayari kufanya kazi na na mtendaji wa kijiji na mtendaji kata Bw, Baruani Gwimo wakidai kuwa alifanya mambo kwa makusudi maana yeye ni mwenyekiti kamati ya ardhi ya kata hiyo hvyo mipango yote juu ya ardhi alikuwa anaijua hali inayoonekana kuwa na mianya rushwa

Baadhi ya wananchi  walitaka Bw, Abel Fransisco aweze kusamehewa kosa lake hatua ambayo ilikataliwa na wengi wakidai kuwa vitendo hivyo vimekithili hapa nchini na kuwafanya wananchi kukata tamaa na hawakotayari kuharibu kijiji chao kwa sababu ya mtu mmoja

 Fransisco, anayetuhumiwa kugawa neo hilo ambalo linatwa kuwa ni zaidi heka 100 amesema kuwa yeye alitoa hati hiyo kwa Samsan Kitwe, kwasababu hakuwa na mtu wa kumshirikisha maana wakati huo serikali ya kijiji ilikuwa imeshavunjwa kufuatia uchaguzi wa serikali za mitaa na ofini hapo kulikuwa na maombi hayo akaona ayafanyie kazi

 Kwa upande wake mtendaji wa kata ya Busagara Baruani Gwimo katika kujitetea kwake amesema kuwa yeye hakushiriki kuuza eneo hilo na wala halija uzwa bali samsoni aliomba kuwa anachungia mifugo yake, ila kilichopo ni uonevu

Anayedaiwa kugawiwa eneo hilo bila utaratibu, Bw, Samsoni Kitwe hakuweza kupatikana na kwenye mkutano huo hakuwepo kwa madai kuwa alipata dahrula iliyomlazimu kusafiri

Hata hivyo wananchi walimtaka akubali makosa yake ili hata siku nyingine aweze kujirekebisha na kama Bw, Kitwe aliomba kuchunga mifugo yake na hati ya kumiliki eneo hilo alipewa yanini?


Kulingana na halivyo, Diwani wa kata hiyo, Godwini Sibanilo alimuagiza mtendaji wa kijijji cha kigendeka kukabidhi ofisi kwa mtendaji wa kata kwakuwa kanuni zina sema hivyo hadi utaratibu wa kupata mtu atakae chukua nafas yake


Halmashauri ya kijiji haina uwezo wa kumuwajibisha mtendaji wa kata bali waliamua kumuandikia mwajili wake amabaye ni mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya  kwa kueleza makosa ya mfanyaka zi wake na kuwa hawako tayari kufanya kazi nae

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya kibondo Bw Judathadius Mboya alipofuatwa kuzunguzia swala hilo alikisema yeye ana majukumu ya kazi maalumu hivyo hana muda kwasasa



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao