Wahitimu jkt muwe mabalozi wema kwenye jamii


Wahitimu jkt muwe mabalozi wema kwenye jamii
Issa Machibya Rc Kigoma


Mkuu wa mkoa wa kigoma kanali mstaafu isay machibiya amewataka vijana wanao hitimu mafunzo ya jkt kuwa na nidhamu katika jamii na kujiepusha na utumiaji wa madawa ya kulevya pamoja na zinaa ilikuendelea kuimalisha afya zao.

Kauli hiyo ameitoa wakati akifunga mafunzo ya kijeshi operation miaka 50 ya muungano mujibu wa sheria kundi la pili katika kikosi cha jeshi 824 kj kilichopo Kanembwa wilayani kakonko mkoani kigoma

Bw.Machibiya amesema idadi kubwa ya vijana imekuwa ikijihusisha  katika matukio mawili hatalishi ikiwa ni pamoja na utumiaji wa madawa ya kulevya pamoja na zinaa ambavyo vimemaliza vijana wengi wakiwa nguvu kazi ya taifa.


Nao vijana waliohitimu mafunzo hayo ya awali kwa mujibu wa sheria  wakiapa mbele ya mkuu wa mkoa na viongozi mbalimbali sambamba na wananchi wameahidi kulitumikia taifa kutokana na mafunzo waliyo pata ilikuhakikisha nchi inaenderea kuwa ya amani upendo na utulivu


Katika Liasra yao vijana hao waliokuwa wakihitimu mafunzo hayo iliyosomwa na Happynes wilison, walieleza changamoto zinazowabili kikosini ikiwa ni ukosefu wa gari la kubeba wagonjwa hali inasababisha usumbu mara wanapopatikana wagonjwa ikilinganishwa na idadi watu waliopo kwenye eneo hilo.


Aidha waliiomba serikali kuongeza muda wa mafunzo uongezwe iwe miezi sita badala ya miezi mitatu inayotumika sasa ili kuwaweka vijana katika hali nzuri zaidi katika kulitumikia Taifa.

Hata hivyo mkuu wa kikosi hicho cha 824 kj kanembwa jkt Luten Kanal Castory Bwegoge amesema kuwa vijana walioanza ni vijana 1333   waliomaliza mafunzo elf 1 miamoja 27 wavulana wakiwa mia 7 stini na2 na wasichamia3 stini 65 wengine 206 walishindwa kumaliza kwasababu mbalimbali ikiwa vifo na matatizo ya kiafya,  ambapo wengi wa wahitimu hao ni walimu wa stashahada, cheti, waliomaliza kidato cha sita

Aidha Bwegoge ameleza kuwa pamoja na changamoto zilizopo, lakini vijana wamejifunza mambo mbalimbali ikiwa ni kushiriki katika shuguli za kijamii  kazi za ujenzi wa taifa kama kushiriki katika ujenzi wa majengo ya maabara katika shule za sekondari wilayani


Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao