Steven Gerrard kuihama Liverpool

Nahodha wa timu ya Liverpool ya Uingereza Steven Gerrard ataondoka katika klabu hiyo wakati mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu.
Gerrard, mwenye umri wa 34, alikuwa huru kusaini makataba wa awali na timu ya nje siku ya Alhamisi na anaaminika kutatakiwa na vilabu vya Marekani.
Gerrard, ambaye alianza kuichezea Liverpool mwaka1998, hatahamia katika klabu nyingine ya Uingereza.
Liverpool ilimpa Gerrard mkataba mpya mwezi Novemba na atatoa taarifa kuhusu mustakhabali wa maisha yake ya soka Ijumaa.
Rais wa klabu ya LA Galaxy ya Marekani Chris Klein amekataa kusema lolote kuhusu klabu yake kumsajili Gerrard, ambaye alifunga penalti mbili katika matokeo ya sare ya 2-2 na timu ya Leicester City katika mechi iliyochezwa siku ya Mwaka Mpya 2015.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Shule ya msingi Nengo ya Walemavu, iliyoko wilayani Kibondo mkoani kigoma, inayohudumia wanafunzi walemavu wa mahitaji maalum inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni ukosefu wa maji Vifaa vya kujinfunza na kufundishia na vyombo vya kulia chakula