Timu ya Nyarugusu juu

Michezo
 Mwemezi Muhingo
Nyarugusu fc yaivunda Kasana fc mikwaju ya mabao 4 kwa 0 wakati wa kusherekea mwaka mpya 2015 mechi iliyochezwa katika uwanja wa mpira wa miguu kata ya mabamba wilayani kibondo mkoani kigoma.

Akizungumza na gazeti la mwananchi Msimamizi wa ligi ya mwaka mpya Bw.Jamal Abdala Tamimu aliesema wameamua kuanzisha ligi ya mwaka mpya kwa lengo la kuwakutanisha vijana wa kata ya mabamba na wananchi ilkikusherekea mweaka mpya 2015

Aidha    Bw.Tamimu amesema michezo ikiwa ni ajila binafsi kwa vijana ameamua kuanzisha mashindano ya mara kwa mara ilikuwaweka vizuri vijana kisoka na kuwaepusha kutumia mda mwingi wakiwa katika magenge na mijadala ambayo haina tija ya maendeleo kwao.

Katika kusherekea sikuu ya mwaka mpya kumechezwa michezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na riadha,mpira wa pete,voribal,mpira wa miguu,na michezo mingine yote ikiwa na rengo la kudumisha michezo na kuwawerka wananachi pamoja.

Hapo Jan1 timu ya nyaruugusu fc ilishuka dimbani kumenyana na timu yak asana fc ambapon kasana fc ilichezea kichapo cha magoli manee kwa mtungi,goli la kwanza lilipatikana dakika ya 18 baada ya mchezaji wa timu ya kiasana Bw.Jonh Misigalo kujifunga mwenyewe huku bao la pili likipatikana dakika ya 43 kupitia kwa Michel Innoncent,hadi kipindi cha kwanza kinatamatika nyarugusu ilikuwa na magoli mawili.


Kipindi cha pili cha mchezo dakika ya 74 Adolfu Nikolausi aliipatria bao la 3 huku Musa Bakari akiipatia bao la nne,michezo hiyo yote inatarajia kukamilika Jan3 kwa michezo ya fainali ilikuwapata washindi 1,2,3 na kuweza kujinyakuria fungate katika michuano hoyo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao