Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2015

UCHAGUZI MKUU: Mwezi mgumu kwa Lowassa

Picha
Dar es Salaam.  Kinyang’anyiro cha kuwania urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) kitafikia katika hatua ngumu mwezi ujao kitakapochukua uamuzi mgumu dhidi ya baadhi ya makada wake walioonyesha nia ya kuwania urais, akiwamo Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa. Kiongozi huyo pamoja na makada wengine sita wa CCM, walipewa kifungo cha miezi 12 kwa madai ya kuanza kampeni za urais mapema kinyume na taratibu za chama hicho iliyomalizika katikati ya mwezi uliopita na sasa wanasubiri kwa hamu, tangazo la Kamati Kuu (CC-CCM) ili wawe huru kutangaza nia ya kuwania urais kwa tiketi ya chama hicho na kuendelea na shughuli nyingine za kujiandalia mazingira ya kupitishwa. Mbali ya Lowassa, wengine waliofungiwa ni Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye; Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja; Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira; Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe; na Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia, January Makamba. Habari kut

Matokeo ya uchaguzi Nigeria leo jioni

Picha
Mkuu wa Tume Huru ya Uchaguzi nchini Nigeria amesema anatumaini kumtangaza mshindi wa uchaguzi wa rais nchini humo ifikapo Jumatatu jioni. Upigaji kura uliendelea katika siku ya pili ya uchgaguzi baada ya kutokea hitilafu katika kadi za kielektroniki na kuchelewesha usajili wa baadhi ya wapiga kura. Bwana Jega amesema alitumaini jumuia ya kimataifa inaweza kupongeza namna Nigeria ilivyoendesha uchaguzi."Tunaamini tumefanya vizuri kabisa. Hatuwezi kupuuza changamoto tulizokumbana nazo. Ni hakika haukuwa kamilifu lakini tunaamini kwa ujumla tumefanya vizuri sana, japokuwa bado tunayo nafasi ya kuzidi kuuboresha. Na kwa namna yoyote ndiyo maana tuliwaalika waangalizi vikiwemo vyombo vya habari na waangalizi wengine wa uchaguzi, ili kuweza kutangaza habari na tunaweza kujifunza kutokana na ripoti hizi na tunaweza kuendelea kuboresha mchakato wa uchaguzi.", amesema Jega. Wachambuzi wa mambo wanasema ushindani ni mkubwa sana kiasi cha kushindwa kutamka mshindi ni nani. Ujumbe wa

Waziri wa Kilimo Kenya amejiuzulu

Picha
Waziri wa Kilimo nchini Kenya Felix Kosgey amejiuzulu baada ya kutajwa katika ripoti ya Tume ya kupambana na ufisadi, akituhumiwa kuhusika na ulaji rushwa katika Wizara hiyo Akizungumza na wanahabari jijini Nairobi, Kosgey amesema ameamua kuachia wadhifa huo baada ya agizo la rais Uhuru Kenyatta juma hili kuwataka maofisa wote wa serikali waliotajwa katika ripoti hiyo aliyoiwasilisha bungeni kujiuzulu. Kosgey amesema binafsi hailewi ni tuhma zipi za ufisadi anazotuhumiwa kuhusika katika wizara hiyo ya Kilimo, na uamuzi wake wa kuachia wadhifa huo pia unatokana na kuheshimu Katiba ya nchi inayomtaka mshukiwa yeyote ambaye ni Ofisa wa serikali anayetuhumiwa kuhusika na ufisadi kuachia ngazi na kuruhusu uchunguzi dhidi yake kufanyika. “Sijui nimehusika na kashfa ipi ya ufisadi, lakini kwa sababu nimetajwa katika ripoti hiyo naachia ngazi nichunguzwe,” alisema. Aidha, amesisitiza kuwa ana uhakika hana kosa na uchunguzi dhidi yake utaonesha hilo na ukweli kubainika. “Jumat

USHAWISHI: Lowassa amponza profesa wa Udom

Picha
Dar es Salaam. Profesa wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Peter Kopoka amebanwa na uongozi wa chuo hicho kutokana na kushiriki maandamano ya kwenda nyumbani kwa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kumshawishi achukue fomu ya kugombea urais. Profesa huyo akiwa na wahadhiri pamoja na watu wengine walioelezwa kuwa ni wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Dodoma walifanya maandamano hayo Machi 22, mwaka huu. Kutokana na tukio hilo, uongozi wa Udom umemtaka ajieleze kwa nini ameshiriki harakati hizo za kisiasa huku akijua kuwa ni mtumishi wa umma anayepaswa kuwahudumia watu wenye itikadi tofauti. Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Idris Kikula alisema kwa kuwa jambo hilo lilionekana kukiwakilisha chuo katika masuala ya siasa, uongozi ulilazimika kumhoji mhadhiri huyo. “Ametuandikia barua ya kujieleza na kubainisha kuwa alikwenda yeye binafsi na siyo kama mwakilishi wa chuo. Lakini mambo haya ni magumu sana kutofautisha. Mimi kwa mfano, siwezi kwenda sehemu halafu nikasema

Saudia yawaondoa raia wake Yemen kusiniVyombo vya habari nchini Saudi Arabia vinasema kuwa nchi hiyo imewahamisha raia wake na wanadiplomasia wa kigeni kutoka mji wa bandari ya Aden kusini mwa Yemen. Jeshi la wanamaji la Saudi Arabia liliongoza oparesheni hiyo. Kundoka kwa watu hao kunajiri wakati waasi wa Houthi wanazidi kuelekea mji wa Aden. Saudi Arabia iliongoza mashambulizi ya siku tatu dhidi ya waasi hao wanaoungwa mkono na Iran lakini hayo yote yameshindwa kuwazuia kusonga mbele Wakaazi wameeleza kuwepo kwa mashambulizi makubwa ya angani kwenye mji mkuu wa Yemen, Sanaa.Vyombo vya habari nchini Saudi Arabia vinasema kuwa nchi hiyo imewahamisha raia wake na wanadiplomasia wa kigeni kutoka mji wa bandari ya Aden kusini mwa Yemen. Jeshi la wanamaji la Saudi Arabia liliongoza oparesheni hiyo. Kundoka kwa watu hao kunajiri wakati waasi wa Houthi wanazidi kuelekea mji wa Aden. Saudi Arabia iliongoza mashambulizi ya siku tatu dhidi ya waasi hao wanaoungwa mkono na Iran lakini hayo yote yameshindwa kuwazuia kusonga mbele Wakaazi wameeleza kuwepo kwa mashambulizi makubwa ya angani kwenye mji mkuu wa Yemen, Sanaa.

Picha
Vyombo vya habari nchini Saudi Arabia vinasema kuwa nchi hiyo imewahamisha raia wake na wanadiplomasia wa kigeni kutoka mji wa bandari ya Aden kusini mwa Yemen. Jeshi la wanamaji la Saudi Arabia liliongoza oparesheni hiyo. Mji wa kusini wa bandari ya Aden nchini Yemen Kundoka kwa watu hao kunajiri wakati waasi wa Houthi wanazidi kuelekea mji wa Aden. Saudi Arabia iliongoza mashambulizi ya siku tatu dhidi ya waasi hao wanaoungwa mkono na Iran lakini hayo yote yameshindwa kuwazuia kusonga mbele Wakaazi wameeleza kuwepo kwa mashambulizi makubwa ya angani kwenye mji mkuu wa Yemen, Sanaa.

Mtandao wa tume ya uchaguzi waingiliwa

Picha
Huku mamilioni ya raia wa Nigeria wakipiga kura kumchagua rais mpya,tovuti ya tume ya uchaguzi nchini Nigeria imeingiliwa na wahalifu wa mtandaoni. Kundi linalojiita Jeshi la mtandaoni la Nigeria limeweka ujumbe katika tovuti hiyo likiionya tume ya uchaguzi ya Nigeria dhidi ya kufanya udanganyifu katika uchaguzi huo. kufikia sasa haijulikani iwapo wahalifu hao wameingia zaidi ya mtandao huo ijapokuwa wamesema kuwa walikuwa wakithibiti data yote ya tume ya uchaguzi. Tume hiyo imesema kuwa ina maelezo kuhusu shambulizi hilo la mtandaoni na sasa imeanza kufanya uchunguzi. Ujumbe huo wa wahalifu hao wa mtandaoni pia unasema kuwa wameweza kuingilia data ya serikali. Mitandao kadhaa maarufu ya serikali ya Nigeria imefungwa katika miaka ya hivi karibuni ukiwemo ule wa bunge. Mtandao wa tume ya uchaguzi nchini Nigeria waingiliwa

Baba mbaroni kwa kuwabaka watoto wake

Picha
Mkazi mmoja wa Miembe Saba wilayani Kibaha mkoani Pwani amekamatwa na polisi akituhumiwa kuwabaka watoto wake wawili wadogo kwa zaidi ya miaka miwili sasa. Habari zilizolifikia gazeti hili, zilisema kuwa katika tukio hilo ambalo limethibitishwa na polisi na watoto wenyewe, baba huyo alianza kuwafanyia binti zake vitendo hivyo mwaka 2013 kwa siku ambazo mkewe ambaye nimama wa wasichana hao hakuwapo hadi usiku wa Machi 19, mwaka huu. Kwa sasa tunayahifadhi majina ya familia hiyo. Watoto hao mmoja mwenye umri wa miaka 15 anayesoma darasa la saba na mdogo wake mwenye umri wa miaka 11 aliyeanza kubakwa akiwa darasa la tatu. Kwa mujibu wa watoto hao, baba huyo alikuwa anamuita mmoja wa watoto wake chumbani kwake na kumtaka alale na mdogo wao wa kiume wakati huo akiwa na mwaka mmoja na binti akipitiwa na usingizi humvua nguo za ndani na kumwingilia huku akimtaka kukaa kimya na kuvumilia maumivu. Mke wa mtuhumiwa huyo, ambaye amekuwa akizimia mara kwa mara kutokana na kulia b
Picha
Dar es Salaam.   Wakati wenyeviti wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) pamoja na kamati zake za kitaalamu wanakutana Zanzibar kutafuta suluhu kuhusu mgawanyo nafasi za kugombea katika uchaguzi mkuu ujao, kuna uwezekano mkubwa vyama hivyo kuteua mgombea urais kutoka Chadema. Tovuti hii inaweza kuripoti kwa uhakika kuwa uwezekano huo unatokana na vigezo vinavyotumiwa na vyama hivyo kusimamisha mgombea mmoja kwa kila jimbo na kwenye nafasi ya urais ambavyo vinaipa Chadema nafasi hiyo dhidi ya vyama vingine katika umoja huo ambavyo ni CUF, NCCR-Mageuzi na NLD. Vigezo hivyo ni matokeo ya uchaguzi 2010, idadi ya madiwani kwa kila chama, matokeo ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Desemba mwaka jana, mtandao wa chama nchini na nguvu ya mgombea iwapo Chadema kitamsimamisha katibu mkuu wake, Dk Willibrod Slaa kwa mara ya pili. Taarifa zilizolifikia Mwananchi kutoka ndani ya kamati ya ufundi ya Ukawa zinasema pamoja na kuwapo mvutano katika baadhi majimbo Ta
Picha
Ndege za kivita mapema leo zilishambulia ngome ya waasi wa Houthi karibu na Ikulu ya Rais wa Yemen mjini Sanaa. Mashambulio hayo yanayoongozwa na majeshi ya Saudi Arabia yanajaribu kukomesha nguvu za kundi la waislamu WaShia-Houthi katika taifa hilo, lililoko katika rasi ya Arabian. Shambulio jingine lilisambaratisha kabisa zana za kivita zilizokuwa katika kituo kimoja cha kijeshi. Mapema leo ijumaa alfajiri, mashambulio kadhaa kusini mwa mji mkuu Sanaa, yaliharibu kituo cha jeshi la aliyekuwa rais wa zamani wa nchi hiyo Ali Abdullah Saleh, mshirika mkuu wa kundi la Houthi. Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Yemen, amesema kuwa mashambulizi ya angani yanayotekelezwa na Saudi Arabia dhidi ya waaasi wa Houthi, yanafaa kusitishwa mara moja. Akiongea na BBC kutoka mji wa Sharm El Sheikh, Bwana Riyadh Yasin anasema kuwa kampeini hiyo ya mashambulio yanafaa kusimamishwa katika kipindi cha siku kadhaa au hata masaa machache yajayo, ikiwa vita vya waasi wa Houthi vitasimamishwa.

Uchaguzi wa Rais: Wanigeria kuamua kesho

Picha
Raia wa Nigeria kesho wanatarajiwa kujitokeza katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo Hata hivyo kumekuwa na vute ni kuvute huku kuripotiwa taarifa ya Mtendaji Mkuu wa Kampuni inayosambaza mashine za kusoma vitambulisho vya elekroniki vya wapiga kura kukamatwa na maafisa usalama wa nchi hiyo. Chama kinachotawala nchini humo cha PDP kimesema kwamba mtendaji huyo Musa Sani anahusishwa na chama kikuu cha upinzani nchini humo cha APC ambaye anadhaniwa kutaka kuvuruga uchaguzi huo. Wagombea Urais Nigeria

Zitto ataja sababu za kujiunga ACT, asema hakuna kurudi nyuma

Picha
Dar es Salaam. Ongeza kichwa  Aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ametaja sababu tano za kujiunga na chama cha ACT-Tanzania huku akijigamba kuwa yeye ni mchapakazi na kwamba sasa mambo yote ni mbele kwa mbele. Akimnukuu Rais wa zamani wa Ghana, Hayati Kwame Nkrumah aliyewahi kusema, ‘forward forever, backward never’, jana Zitto alisema, sasa ni wakati wa kuangalia mbele, hakuna kurudi nyuma tena huku akijisifu kwa umahiri wake katika kazi. “Mimi ni mchapakazi…siangalii nyuma tena, naangalia mbele . Mapambano yanaanza matokea mtayaona baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu,”alisema Zitto kujiamini. Zitto ambaye aling’atuka kutoka kwenye nafasi ya Ubunge  Ijumaa iliyopita kupitia Chadema na kujiunga na chama ACT siku moja baadae, alisema watu wengi wamekuwa nini kingefuata baada ya ya kuachia nafasi . “Sasa napenda kuwaarifu kuwa Machi 20, mwaka huu siku ya Jumamosi nilijiunga na chama cha ACT na kukabidhiwa kadi ya uanachama na mwenyekiti ACT,  Tawi la

IS yataka Wanajeshi 100 wa US wauwawe

Picha
Jeshi la Marekani linasema kuwa linawajulisha karibia wanajeshi 100 waliotajwa kwenye orodha ya mtandao ulionzishwa na Islamic State unaotaka wauawe. Kitengo cha kudukua mitandao cha Islamic State kinawataka wale wanaolipendelea kundi hilo kuwaua wale walio kwenye orodha hiyo ambao Islamic State inawalaumu kwa kuendesha mashambulizi ya angani dhidi yake nchini Iraq na Syria. Majina yao, picha na namba zao zimechapishwa kwenye mitandao. Kitengo cha ujasusi cha jeshi la wanamaji la Marekani kinasema kuwa tishio hilo halijathibishwa rasmi . Kitengo hicho kinawataka wanajeshi kuchukua tahadhari kuhusu ujumbe unaowahusu wanaoweka kwenye mitandao. Jeshi la Marekani linasema kuwa limeanza kuwajulisha wanajeshi 100 wa Marekani waliotajwa katika mtandao wa IS unaotaka wauawe

Wanajeshi watoto waachiliwa Sudan Kusini

Picha
Waasi nchini Sudan Kusini wamewaachilia huru wanajeshi watoto wapatao 250 . Ni oparesheni ya tatu katika msururu wa hatua zilizoanza kuchukuliwa na jeshi hilo mnamo mwezi Januari. Mpango huo unatokana na makubaliano ya amani yaliotiwa sahihi mwaka uliopita kati ya serikali na waasi katika jimbo la Jonglei wanaojulikana kama Kobra. Shirika la watoto la umoja wa mataifa UNICEF ambalo linasaidia katika operesheni hiyo limesema kuwa watoto wengine 400 zaidi pia wataachiliwa huru katika kipindi cha siku chache zijazo na kuifanya kuwa idadi kubwa ya watoto wanajeshi walioachiliwa kufikia sasa. Hatahivyo UNICEF limesema kuwa kuna takriban wanajeshi watoto 12,000 wanaohusishwa na mzozo unaondelea kati ya serikali na waasi wanaoungozwa na aliyekuwa makamu wa rais Riek Machar. Wanajeshi watoto

Katiba ni mali ya wananchi, waielewe

Picha
Tunaendelea na mfululizo wa makala haya kuhusu Katiba Inayopendekezwa baada ya kumaliza sehemu ya pili wiki iliyopita. Ni muhimu kuendelea kusisitiza kuwa siyo sahihi kupigia kura ya “Ndiyo”au “Hapana” Katiba Inayopendekezwa wakati bado haifahamiki kwa wananchi, haijawafikia wananchi na bado muda wa kuelimisha kwa umma ni mfupi kumwezesha kila mtu kuisoma, kuichambua, kuielewa na kuitumia. Tunaendelea kusisitiza tena kuwa kila mtu ana haki na anastahili kuijua, kuisoma ama kuelimishwa na kuwa na nakala yake ili kwa wakati wake ajisomee binafsi kwa uelewa zaidi. Tunaendelea kusisitiza tena kuwa idadi ya nakala zilizotolewa hazikidhi haja ya kuwahabarisha, raia walio wengi kuijua, kuielewa na kuitumia Katiba hii kwa minajili ya kuipigia kura. Tunaomba na kuitaka mamlaka husika kutuchukulia sote kuwa tuna haki na wajibu wa kuijua, kuielewa, kuichambua na kisha kuipa uhalali ama kuikataa kwa hoja za uhakika. Mjadala wa wiki hii katika kipindi cha Malumbano ya Hoja kinacho

Mgonjwa wa Ebola Yardolo akituhusiwa kwenda nyumbani

Picha
Kisa kipya cha ugonjwa wa ebola kimegunduliwa nchini Liberia wiki chache kabla ya nchi hiyo kutangazwa kuwa isiyokuwa na ugonjwa huo. Mkuu wa kundi linalohusika na kudhibiti ugonjwa wa ebola nchini humo ameiambia BBC kuwa mwanamume mmoja ambaye alipelekwa kwenye kituo cha matibau siku ya alhamisi alipatikana akiwa na ugonjwa wa ebola. Wiki mbili zilizopita mgonjwa wa mwisho wa ugojwa wa ebola (Beatrice Yardolo) aliruhusiwa kuondoka hospitalini kwenye mji mkuu wa nchini hiyo Monrovia. Liberia ilikuwa imesalia na siku 40 kabla ya kutangazwa kuwa isiyo na ugonjwa wa ebola kulingana na taratibu za shirika la afya duniani WHO. Zaidi ya watu 4000 wameaga dunia nchini Liberia kutokana na ugonjwa wa ebola.

IS yakiri kushambulia misikiti Yemen

Picha
Kundi la Islamic State linasema kuwa wapiganaji wake waliendesha mashambulizi ya kujitoa mhanga kwenye misikiti miwili nchini Yemen ambapo zaidi ya watu 130 waliuawa. Washambuliaji wanne wa kujitoa mhanga walilenga waumini kwenye mji mkuu Sanaa wakati wa maombi ya Ijumaa. Maeneo hayo mawili hutumiwa na waumini wanaowaunga mkono waasi wa Shia wanaofahamika kama Houthi ambao walichukua udhibiti wa mji wa Sanaa mwaka uliopita. Zaidi ya watu 200 walijeruhiwa wakati wa mashabulizi hayo ambapo wito wa kuwaomba watu kutoa damu umekuwa ukitolewa. kundi la wapiganaji wa IS limekiri kutekelza ,mashambulizi katia misikiti ya Yemen

Waliodanganya mtihani wafukuzwa India

Picha
Wakuu wa jimbo la Bihar, India, wamewakamata mamia ya watu na wamewafukuza wanafunzi zaidi ya 750 baada ya video kutanda mtandaoni, zinazoonesha wanafunzi wakidanganya wazi kwenye mtihani wa kumaliza shule. Baadhi ya wazee na askari polisi wamekamatwa, na mitihani ijayo katika vituo vine imeahirishwa. Picha hizo zinaonesha wanaume wakiparamia kuta za vituo vya mitihani na kuwakabidhi wanafunzi majibu, na wanafunzi wengine wakikopi kutoka maelezo hayo.

Utandawazi, umasikini wa kipato katika familia na tamaa mbaya chanzo cha mimba za utotoni kwa wanafunzi wa shule sekondari na msingi

Picha
Wanafunzi wa shule ya sekondari Bishop Mpango iliyoko Kibondo Utandawazi, Umasikini wa kipato katika familia, ukosefu wa maadili ya utumishi Mila na destuli na Tamaa za vitu vidogovidogo vimetajwa kuwa ni vyanzo vya kuwepo kwa mimba za utotoni, kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari pamoja na watoto walioko mitaani. Hayo yamesemwa na Baadhi ya Wanafunzi wa shule hizombalimbali, Wilayani Kibondo mkoa wa kigoma, walipokuwa wakiongea na Muhingo Blog jana kwa nyakati tofauti mjini humo. Waamesema kuwa umasikini   ni chanzo kikubwa hasa kwa wanafunzi wa shule za sekondari wakutwa kwa kutoishi Bweni kwani muda mwingi uwa mitaani na wengine kutopata chakula na mahitaji muhimu hali inayowapeleka katika vishawishi na kujikuta wametumbukia katika kufanya ngono na kubeba mimba katika umri mdogo Hata hivyo,   waliweka wazi kuwa wapo walimu ambao nao wamekuwa wakiwasumbua wanafunzi mashuleni kwa kutaka wafanyenao mapenzi nakuwalagai kwa kuwapa vitu vidogovid

Wanawake Kibondo, jiepusheni na kurubuniwa na vitu vidogovidogo katika uchaguzi 2015

Picha
Wito umetolewa kwa madhehebu yote kuendelea kuliombea taifa hasa wakati huu wa uchaguzi ambapo vitendo vya kikatili hasa mauaji ya albino vinavyo jitokeza kwa imani za kishilikina. Kauli hiyo, imetolewa na Bi Juster Paulo mkazi wa Urambo mkoani Tabora, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya maombi kwa wananwake duniani ambayo yaliandaliwa na umoja wa wananwake CCT Wilaya ya Kibondo mkoani kigoma, kwa lengo la kuungana pamoja na kuliombea taifa, ambayo yalifanyika jana katika Kanisa la Kiijili la Kiluthel Tanzania KKKT . Bi. Juster  amesma viongozi wanao wania nyazifa mbalimbali ndani ya serikali wanatajwa kujihusisha na imani za kishilikina ambapo kila ikariibiapo muda wa uchaguzi hujitokeza mauaji ya albino na hivyo Wakristo na watanzania wote  hawana budi kuungana na kuliombea taifa dhidi ya mauaji hayo. Aidha amewataka wanawake kote nchini kuacha tabia ya kuendekeza kupewa viu vidogovidogo na baadhi watu wanaogombea nafasi mbalimbal