Utandawazi, umasikini wa kipato katika familia na tamaa mbaya chanzo cha mimba za utotoni kwa wanafunzi wa shule sekondari na msingi

Wanafunzi wa shule ya sekondari Bishop Mpango iliyoko Kibondo


Utandawazi, Umasikini wa kipato katika familia, ukosefu wa maadili ya utumishi Mila na destuli na Tamaa za vitu vidogovidogo vimetajwa kuwa ni vyanzo vya kuwepo kwa mimba za utotoni, kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari pamoja na watoto walioko mitaani.

Hayo yamesemwa na Baadhi ya Wanafunzi wa shule hizombalimbali, Wilayani Kibondo mkoa wa kigoma, walipokuwa wakiongea na Muhingo Blog jana kwa nyakati tofauti mjini humo.

Waamesema kuwa umasikini  ni chanzo kikubwa hasa kwa wanafunzi wa shule za sekondari wakutwa kwa kutoishi Bweni kwani muda mwingi uwa mitaani na wengine kutopata chakula na mahitaji muhimu hali inayowapeleka katika vishawishi na kujikuta wametumbukia katika kufanya ngono na kubeba mimba katika umri mdogo

Hata hivyo,  waliweka wazi kuwa wapo walimu ambao nao wamekuwa wakiwasumbua wanafunzi mashuleni kwa kutaka wafanyenao mapenzi nakuwalagai kwa kuwapa vitu vidogovidogo na hatimae kuwapachika ujauzito, ikiwa ni pamoja na utandawazi kama wanavyoeleza  Lidia Ladslaus na Enock Arcado wanafunzi.
Walieleza kuwa wapo  baadhi ya  watumishi wa afya  ambao ufanya kazi za kuwatolea mimba watoto na kusababisha kutokuwepo na hofu miongoni mwao japo ni hatari  kwa maisha yao huku baadhi ya wanafamilia kutengeneza mahusiano ya kindugu kwa kuwalazimisha vijana wao hata kama wana umri mdogo kuwaoza pasipo kujali  kama wanasoma shule  walieleza Hadija Shija na Nomi Maulidi wanafunzi wa Bishop 
Mpango shule ya sekondari

Helieth Samweli, ni mwalimu katika shule ya sekondari ya Mpango, alisema kuwa lipo tatizo kwa walimu ambao wanaajiliwa wakiwa na umri mdogo ambapo wanapofika mashuleni ujikuta wanaanzisha mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi hali ambayo uchangia kushuka kwa kiwango cha elimu na mimba za utotoni, huku mwalimu Chizero Bungubuliho, ambaye mkuu wa shule ya Maragalasi  anasema kuwa wanafunzi wanaobeba ujauzito kwa kiwango kikubwa ni wale wakutwa kwasababu ukaa muda mwingi mitaani tofauti na wale wa Bweni 

Nae Afisa Elimu wa shule za Sekondari wilayani kibondo Bi, Honoratha Kabundugulu, amekili kuwepo kwa tatizo la baadhi ya walimu kufanya mapenzi na watoto wa shule,  hatua aliyoitaja kuwa chanzo  ni tatizo la ajira, hivyo vijana wengi uingia katika taaluma ya  ualimu bila kufuata maadili ya kazi na kuwafanya maafisa elimu badala ya kuwalea wanafunzi, ugeuka na kuwa walezi wa walimu.

Mmoja wa wazazi Bw, Julias Bunyambo, mkazi wa kibondo alikataa malalamiko ya watoto hao si sahihi kwani kipindi hiki watoto wengi wanakumbwa na mmomonyoko wa maadili na kuwa na tamaa zisizokuwa za msingi hata kama wanapatiwa huduma zote  na kuwataka kuwa  kwani yeye anawatoto wa kike ambao amekuwa akiwapa huduma zote lakini walibeba ujauzito mashule na sasa anafanya kazi ya kulea wajukuuna mama zao, na kuwataka  wanafunzi watulivu na kuvumilia hadi watimize ndoto zao kwani hata watu wazamani walisoma .

Blog hii, ilifika katika Hospitali ya wilaya ya Kibondo na kuongea na Mratibu wa Afya ya uzazi wa wilaya Bi Edna Lymo ambaye anaeleza kuwa kumekuwepo na changamoto ya mimba za utotoni lakini tatizo kubwa kutokuwepo na uelewa katika jamii na watoto wenyewe juu ya afya ya uzazi kwa sababu wizara ya Afya na wizara ya Elimu hawajakaa pamoja na kuweka utaratibu ili elimu ya afya ya uzazi ifundishwe mashuleni kwa kuhofu kuwepo uharibifu mkubwa.

Wilaya ya Kibondo tangu mwezi Oktoba mwaka jana 2014 hadi sasa imekuwa na wanafunzi watoro wa kudumu hasa kwa shule za msingi wapatao  2800 ambapo wanaobeba ujauzito uamua kutoroka kabla kabainika na kuchukuliwa hatua za kinidhamu.
Mwisho

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao