Kiwango cha Elimu hakipandi mkoani Kigoma kwa muda mrefu

Mkoa wa Kigoma umekuwa ukifanya vibaya kaika Mitihani ya Darasa la saba kwa kushika nafasi ya 24 kati ya mikoa 25 kwa kupiga hatua ya asilimia 1 tu na ushindi wa asilimia 42 hali iliyotajwa kuwa ni mbaya katika ukuaji wa kiwango cha  Elimu

Hayo yamesemwa na madiwani wa Halmasahauri ya wilaya ya Kibondo mkoani humo wakati wa kikao cha baraza cha robo ya pili kilichofanyika mjini humo, ambapo wamedai kuwa wilaya hiyo imekuwa ikishika nafasi ya 5 kati 7 kwa miaka 5 mfululizo

Madiwani  hao wametaja baadhi ya mambo yanayosababisha kuwa ni pamoja na Walimu kuchelewa kufika makazini,Baadhi ya walimu kuchelewa kutoka likizoni,Wanafunzi kutokuwa na maandalizi ya kutosha kabla ya kuingia madarasani, ulevi wa kupindukia, mwamko mdogo wa jamii katika elimu na Baadhi ya Walimu wa muda mrefu makazini kuwatishia maisha waratibu elimu wa kata mbalimbali mara wanapotakiwa kufanya ukaguzi katika maeneo yao ya kazi


Afisa elimu wa wilaya hiyo, Joseph Tirutangwa amekana kuwa waratibu elimu wa kata haleti taarifa zilizo sahihi kwa sababu ya kutishiwa maisha na baadhi ya wlimu ila kinachotakiwa kwa madiwani hao kufika katika ofisi za elimu na kupata ufafanuzi wa yale wanayokuwa nawasiwasi nayo ila kwa swala la kushuka kwa elimu hiyo ni Historia ya wilaya hiyo na siyo kwa sasa maana nyakati maafisa elimu wote wilayani humo wanasambaa vijijini ili kufanya ukaguzi na kuona hali halisi ilivyo
]

Hata hivyo Tirutangwa amedai kuwa ushindi wa asilimia 42%  wa mkoa wa Kigoma siyo mzuri ila  kinachotakiwa ni jamii  wazazi na  Walimu kushirikiana kwa pamoja ili kuinua kiwango cha elimu na pia hawatakiwi kukata tama na wao najaribu kuwapa stahiki zao kwa wakati jinsi serikali inavyoleta fedha


Hata hivyo mmoja wa Waratibu elimu kata,  wilaya humo Bi ………………  amaesema kuwa yawezeakana  mambo hayo yakawakumba  wenzake  ila yeye hajatishiwa na mwalimu yeyeote na wala  jambo haliwezi kusababisha kushuka kwa taaruma


Kwa upande wao baadhi ya walimu wamekataa kuwepo kwa swala  la  kuwatishia Maisha waratibu elimu mara wanapofika kwenye kazi  vyao vya  kazi kukangalia uendaji wao wa kazi  kama taratibu zinavyoelekeza kama anavyoeleza   Edward  Buhanza  shule ya Msingi Kibondo kuwa jambo hilo hata kama lingekuwepo, haliwezi kusabisha kushuka kwa kiwango cha Elimu


Aidha amesema kuwa mambo yanayochangia kushuka kiwango cha elimu ni pamoja  Walimu kuwa na Mikopo yenye riba kubwa, ambayo inawafanya walimu wengi kushindwa kufanya kazi  bidii, Moyo wa kufundisha kwa kujitoa kwa walimu umeshuka kwa kiasi kikubwa  na Fedha za kuendeshea shule  kuchelewa na zikiletwa uwa ndogo hivyo kutokidhi mahitaji kwa sababu walimu ukosa vifaa vya kundishia na kujifunzia

Kwa upande wao baadhi ya walimu walipoulizwa kwanini upenda kujiingiza kwenye mikopo ya ri kubwa na kushindwa kufanya kazi walioajiriwa kwayo, wameeleza kuwa ni kulingana hali ya maisha ilivyo kwa hivi sasa  ikilinganishwa na mishahara ilivyo kama anavyoeleza mwalimu Anna Maulidi toka shule ya msingi Mapinduzi japo anasema kuwa kwa hivi sasa yeye shuleni kwao walianzisha saccos ya shule hivyo jambo hilo haliwaahiri sana

Nae mwanafunzi Lidia Dickson ambaye ni mwanafuzi wa shule ya msingi Mapinduzi aneleza maandalizi yake anayokuwanayo kabla na baada ya kwenda shule  na jinsi anavyoimizwa na wazazi wake kujali masomo kuwa ndo msingi na mwanga wa maisha yake ya baadae

Wananchi wameiomba idara ya elimu ya wilaya hiyo kuhakikisha inaweka usimamizi mzuri kwa kuwa muda mrefu yamekuwepo malalmiko kuwa usimamizi wake hauridhishi ndo sababu wanafunzi wakuwa wakishindwa mara kwa mara kwenye mitihani yao kama anavyoeleza Falesi Magwala mkazi wa Kibondo


Idara ya elimu ilikuwa na wanafunzi ambao ni watoro wa kudumu wapatao 2800 kuanzia mwezi october  mwaka jana  katika shule za msingi na wengi wao uacha masomo na kukimbilia wilayani urambo mkoani Tabora kufanya kazi katika mashamba ya Tumbaku, wengine ukimbilia wilayani Kahama mkoani Shinyanga kufanya kazi za kuchota maji na kuchunga Ng’ombe

                

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao