Kamati ya Bunge yaitia Kiti Moto Halmashauri ya Wilaya Kibondo

Selemani Zed makamu mwenyekiti wa kamati ya Bunge 
Kamati ya Bunge yaitia Kiti Moto Halmasauri ya Wilaya Kibondo


Kibondo,  Kamati ya bunge ya hesabu za serikali za mitaa imeeleza kutoridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi ya Halmashauri ya wilaya Kibondo mkoani Kigoma, kutokana na kuwepo mianya mingi inayoashiria ubadhirifu wa fedha za miradi.

Akitoa majumuisho ya maoni ya wajumbe wa kamati hiyo Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo,Suleiman Zedi ameitaka Halmashauri kutoa taarifa za kina na kuziwasilisha kwa mkaguzi na mdhibiti wa serikali Kigoma ambao wataipatia kamati hiyo taarifa hiyo.

Wakati wa majumuisho yake kwa kamati Mwenyekiti huyo, Zed amesema kuwa kamati imeshangazwa na kitendo cha Halmashauri kushindwa kufunga vifaa vya kusukuma maji kwa zaidi ya miaka 5 wakati vifaa hivyo vipo,kushindwa kuweka chujio la maji na kufanya wananchi wa Kibondo mjini kunywa maji machafu hali ambayo ni hatari kwa afya za binadamu.

Sambamba na hilo Kamati hiyo imeshangazwa na kitendo cha wataalam na wakuu wa idara kutumia kiasi cha shilingi milioni 80 kujilipa posho katika mradi wa ujenzi wa bwawa la umwagiliaji Nyendara huku Halmashauri ikishindwa kujenga mfereji wa kupeleka maji katika mashamba ya wakulima kinyume na malengo yaliyokuwepo. Wakati mradi umegharimu kiasi cha shilingi milioni  zaidi ya 600 Halmashauri ya wilaya ya kibondo imetumia kiasi cha shilingi milioni tatu tu kuchangia katika utekelezaji wa mradi huo.

Mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo Kangi Lugora, amedai kuwa wa Halmashauri haikuwa makini katika matumizi ya fedha za utekelezaji wa mradi huo na kutoa mwanya wa wakuu wa idara na wataalam kujinufaisha ni pamoja na kuwepo wakuu wa idara wakijipa kazi ya kutekeleza mradi huo badala ya kuteua kampuni ya ukandarisi,na malipo ya zaidi ya shilingi 600,000 kwa mtoto mchanga wa mmoja wa watumishi wa Halmashauri hiyo ambaye aliambatana na mama yake kwenye ziara za kikazi.

 Katika majibu yao kwa kamati hiyo wakuu wa idara na wataalam wa Halmashauri hiyo wamekuwa wakishindwa kutoa maelezo ya kuridhisha kuhusiana na matumizi ya fedha za miradi huku wananchi wakishindwa kupata huduma.


Akitoa maelezo kwa kamati hiyo,Kaimu Mhandisi wa maji wa wilaya ya Kibondo,Tandali Matwiga alisema kuwa walilazimika kutekeleza mradi wao wenyewe kutokana na uharaka wa mradi kwa vile wananchi walikuwa na tatizo kubwa la maji. Huku akishindwa kuwa na maelezo ya kutosha ya kushindwa kufungwa kwa mota na pampu kwa ajili ya kusukuma maji kupeleka kwa wananchi.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo, Emili Mpfanye katika kujitetea kwake aliweka wazi kuwa matatito mengi yalitokea wakati wa uongozi uliopita na hadi ukabadilishwa akashika ngazi yeye, pia na wakuu wa idara walio wengi ni wageni. huku Katibu Tawala serikali za mitaa mkoa wa kigoma Moses Msuluzya akiahidi mbele ya kamati kuwa karibu na Halmashauri hiyo ili kuhakikisha mapungufu yaliyobainika yanarekebishwa

Hata hivyo baadhi ya wananchi walipoona kamati hiyo ikikagua chanzo cha maji cha Mgoboka walifika huku Benard Kasuka mkazi wa kijiji cha Kumhama akitoa malalamiko yao juu ya kulipwa fidia ya mazao na mashamba ili waweze kupisha katika eneo hilo na uendelezaji wake uweze kukamilika walikataliwa na kuambiwa hakuna malipo kwani huo ni uhabifurifu, na serikali ilishapiga marufuku kuendesha shuguli za kilimo katika vyanzo vya maji.
Mwisho


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao