Wanawake Kibondo, jiepusheni na kurubuniwa na vitu vidogovidogo katika uchaguzi 2015



Wito umetolewa kwa madhehebu yote kuendelea kuliombea taifa hasa wakati huu wa uchaguzi ambapo vitendo vya kikatili hasa mauaji ya albino vinavyo jitokeza kwa imani za kishilikina.

Kauli hiyo, imetolewa na Bi Juster Paulo mkazi wa Urambo mkoani Tabora, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya maombi kwa wananwake duniani ambayo yaliandaliwa na umoja wa wananwake CCT Wilaya ya Kibondo mkoani kigoma, kwa lengo la kuungana pamoja na kuliombea taifa, ambayo yalifanyika jana katika Kanisa la Kiijili la Kiluthel Tanzania KKKT .

Bi. Juster  amesma viongozi wanao wania nyazifa mbalimbali ndani ya serikali wanatajwa kujihusisha na imani za kishilikina ambapo kila ikariibiapo muda wa uchaguzi hujitokeza mauaji ya albino na hivyo Wakristo na watanzania wote  hawana budi kuungana na kuliombea taifa dhidi ya mauaji hayo.

Aidha amewataka wanawake kote nchini kuacha tabia ya kuendekeza kupewa viu vidogovidogo na baadhi watu wanaogombea nafasi mbalimbali ili waweze kuwachagua kwani hata wanawake wanahaki sawa na watu wengine hivyo hawastaili kudharaliwa wala kujinyanyapa na wanatakiwa kujisimamia utu wao

Kwa upande wao baadhi ya akina mama wamesema ni vema kusikiliza sera za wagombea na kuwapima kwa hotuba zao badala ya kuwa wepesi kupokea zawadi ambazo hazina mashiko katika uongozi wa serikali ili kutengeneza utawala bora ujao katika nchi  alieleza    Bi  Namsifu James mkazi wa kibondo

Siku hii ya Maombi ya Dunia  kwa Wanawake   uadhimishwa kila mwaka katika mwisho wa wiki ya kwanza ya mwezi marchi kabla ya maadhimisho wa siku ya wanawake Duniani ambayo ufanyika mwezi march kila mwaka,  ambapo umoja wa wanawake
wa CCT Kibondo wameadhimisha kwa kuliombea Taifa juu ya uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika October mwaka uhuu uwe wa amani kama alivyosoma lisara ya umoja huo, Bi Melse Bulugu katibu wa umoja wa wanawake

Pamoja hayo wamesema kuwa wanawake wengi wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuachiwa mizigo mikubwa ya kulea na kuhudumia familia na mifumo ya zamani ya wanake kutokupata nafasi ya kupaza sauti zao kuzifanya familia kutopiga hatua katika maendeleo, hayo anayaeleza Bi Sarah Wiliam huku wanaume wanao wakitoa maelezo yao kuwa majukumu ya Baba katika familia hayawezi kufanya  uwenda ndo sababu wakina mama udhani wameachiwa mzigo wa familia peke yao


Sambamba na hilo katika maadhimisho hayo wakina mama hao wao wameshiriki kutoa msahada thamani ya shilingi laki 7ikiwa ni  Sabuni na Mafuta ya kupaka    kwa Wafungwa na maabusu kwenye Gerza la Wilaya Kibondo lengo iikiwa ni kuwafariji binadamu wanaoishishi katika mazingira magumu


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao