Jeshi la Ukraine kuondoka mji wa vita

Rais wa Ukraine Petro Poroschenko amesema kuwa majeshi ya Ukraine yanakaribia kumaliza mipango yake ya kuondoka mji wa Debaltseve kuliko na mapigano.

Picha za runinga zinaonyesha milolongo ya vifaru na magari mengine ya kijeshi pamoja na wanajeshi wakiondoka maeneo hayo.

Bado milio ya risasi na mizinga inasikika licha ya kutiwa saini kwa muafaka wa kukomesha vita na kuondoa silaha nzito nzito toka mji huo kutiwa saini juma lililopita.

Wanajeshi wa Ukraine wakijitayarisha kuondoka mji wa Debeltseve
Rais Poroshenko anasema kuwa kuondoka kwa majeshi yake kumepangwa barabara na amekanusha taarifa kuwa majeshi ya Ukraine, kamwe hayakuwa yamezingirwa.
Sasa anaelekea mashariki mwa taifa ili kuwalaki wanajeshi wake.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao