Ukosefu wa ajira unahatarisha afya za Watanzania

Wapo pia wale wanaostaafu na kujikuta hawajaandaa mazingira mazuri ya kuendelea kuwa na kipato.
Hapa Tanzania ukosefu wa ajira huelezwa kuwa ni hali ya mtu kutokuwa na shughuli inayomuwezesha kupata kipato kitakachomsaidia yeye au pamoja na familia yake katika maisha ya kila siku.
Kutokana na hali hiyo, wenye ajira ni pamoja na wale walioajiriwa au kuajiri kwenye mfumo rasmi au usio rasmi. Asiye na ajira anawekwa katika kundi la wale ambao hana shughuli ya kumpatia kipato.
Hivi karibuni, Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Makongoro Mahanga alinukuliwa akisema ukosefu wa ajira kwa Tanzania umefikia kiasi cha asilimia 12. Kiasi hiki cha watu wasiokuwa na ajira ni sawa na idadi ya watu milioni sita.
Watu wengi wanafikiri kuwa ukosefu wa ajira ni tatizo la kiuchumi pekee, lakini watafiti wa masuala ya afya wanabainisha kuwa hili pia ni tatizo kubwa la afya ya jamii.
Katika utafiti uliochapishwa mwaka huu hivi karibuni katika Jarida la The Lancet Psychiatry, unaonyesha kuwa ukosefu wa ajira unasababisha vifo vya watu wengi duniani.
Utafiti huo ulioongozwa na Dk Carlos Nordt wa Hospitali ya Magonjwa ya Akili katika Chuo Kikuu cha Zurich, Uswisi ulibaini kuwa kati ya mwaka 2000 na 2011, ukosefu wa ajira duniani ulisababisha takriban vifo vya watu 45,000, vilivyotokana na kujiua kila mwaka.
Ripoti za kiuchunguzi kutoka pande mbalimbali za dunia zinaonyesha kuwa, siku za hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la watu wasiokuwa na ajira pia ongezeko la watu wanaojiua au wanaojaribu kujiua.
Utafiti wa Shirika la Afya Duniani
Shirika la Afya Duniani (WHO) katika uchunguzi wake uliochapishwa mwaka 2014, lilibaini kuwa kila sekunde 40 mtu mmoja duniani hujiua na inakadiriwa kuwa watu 800,000 hufa kila mwaka kutokana na kujiua. Hapa nchini tatizo la kujiua ni kubwa kiasi kwamba Tanzania inashika namba ya nane duniani kati ya nchi zinazoongoza kwa watu kujiua.
Ingawa kuna sababu nyingi zinazofanya watu kujiua au kupata madhara ya kiafya hapa nchini, kuna uwezekano mkubwa pia kuwa Watanzania wengi huhatarisha maisha yao kutokana na tatizo la ukosefu wa ajira.


Septemba mwaka jana Ernest Magashi wa Bukombe mkoani Geita aliripoti habari za mtoto mdogo Hadija Deo wa mtaa wa Kapala, Kata ya Igulwa aliyekutwa katika hali mbaya ya kiafya baada ya mama yake Zainabu Selemani kudaiwa kumficha ndani kwa muda mrefu.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao