Bomu lalipuka nje ya ikulu ya rais Yemen

Bomu limelipuka nje ya ikulu ya rais wa Yemen, katika mji mkuu, Sanaa, mji ambao sasa unadhibitiwa na wapiganaji wa madhehubu ya Shia, wa Houthi

Inaarifiwa kuwa waasi wawili wa Houthi walijeruhiwa.
H
Sasa wapiganaji hao wamebuni halmashauri ya usalama kuongoza nchi hadi bunge la muda litakapoundwa.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema kuwa liko tayari kuchukua hatua zaidi, iwapo wapiganaji hao hawatarudi haraka kwenye mazungumzo, kuhusu kipindi cha mpito cha kuelekea kwenye demokrasi.

Ikulu ya rais nchini Yemen
Baraza jiiya limewataka wapiganaji wamuachilie huru rais wa Yemen, waziri mkuu, na baraza la mawaziri kutoka kifungo cha nyumbani.
apo jana wapiganaji hao walilivunja bunge kabla ya kudhibiti madaraka.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao