Afisa Elimu Afariki gafla akiwa ofisini kwake

Afisa Elimu Afariki gafla akiwa ofisini kwake 


Afisa elimu vifaa na takwimu wilayani kibondo mkoani kigoma  bw Jones Biria jana alifariki ghafla akiwa ofisini kwake alikokuwa akiendelea na shughuli zake za kiofisi

Akizungumza kuhusu historia fupi ya kifo cha marehemu afisa elimu wa shule za msingi wilayani kibondo Joseph Tirutangwa amesema kuwa kifo hicho kimetokea jana april 21 majira ya jioni ambapo marehemu alizidiwa ghafla kisha kupoteza fahamu

Aidha akizungumzia mazingira ya kifo hicho bw Tirutangwa amesema kuwa marehemu alikuwa anaongea na mlinzi wakiwa wamekaa kwenye viti vya nje vinavyotumiwa na watu wanaosubiria huduma ndipo marehemu alizidiwa ghafla kisha haraka akamtuma mlinzi akamuite afisa elimu na alipokuja eneo la tukio alikuta tayari ameshaanguka na kupoteza fahamu

Bw Tirutangwa amesema kuwa baada ya hari hiyo kujitokeza marehemu alikimbizwa haraka katika hospitali ya wilaya ya kibondo ambapo kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya kibondo dr Kizito Ruhamvya aliyeufanyia uchunguzi  mwili huo, na kuthibitisha kuwa  kifo cha marehemu kimetokana na shinikizo la damu pamoja na kisukari
Mwili  wa  Afisa Elimu huyo umesafirishwa kwenda Buseresere Wilaya ya Chato mkoani Geita kwa ajili ya Mazishi  


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao