Togo kumchagua rais mpya jumamosi

Wapiga kura nchini Togo watamiminika vituoni kesho Jumamosi kumchagua rais mpya kwa muhula mingine wa miaka mitano. Rais wa sasa Faure Gnassingbe, ndiye anatarajiwa kuibuka mshindi katika ya wagombea watano.
Amekuwa uongozi tangu mwaka 2005 baada ya kumrithi babake ambaye aliitawala Togo kwa miaka 38.
Uchaguzi huo unafanyika licha ya kuwepo malalamiko kutoka kwa upinzani na mashirika ya umma kuhusu kutokuwepo mabadiliko ambayo yatapunguza mihula ya rais.
Upinzani ulilalamikia uchaguzi wa mwaka 2005 na 2010, ukikishutumu chama kinachoongoza kwa wizi wa kura.
Rais wa Ghana na mkuu wa Ecowas Dramani Mahama ambaye aliizuru Togo mara mbili zaidi ya siku 30 zilizopita ametaka kuwepo uchaguzi wa amani.
Gnassingbe Eyadema, babake rais wa sasa aliaga dunia mwaka 2005 baada ya miaka 38 uongozini, baada ya kuingia madaraka kupitia mapinduzi ya kijeshi mwaka 1967.
OnKampeni nchini Togogeza kichwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao