Polis walaumiwa kwa kuwatesa wananchi

Marko Joshua Ocd Kibondo
Hassan Masala Dc Kibondo
Herman Vedasto  mkazi wa kijiji cha Mulungu akilalamika mbele dc kuhusu mateso wanayopewa na polisi


Baadhi ya wakazi wa vijiji vya,Kumhasha kata ya  Mulungu na Bunyambo Kata ya Samvula, wamelilalalimkia Jeshi la polisi wilaya ya Kibondo mkoa wa Kigoma kwa kile walichokitaja kuwa ni unyanyasajia dhidi ya Raia wasiyokuwa na hatia

Hayo wamewekwa na wananchi hao, wakimwambia mkuu wa wilaya hiyo, Bw, Hassani Masala mara alipotembea vijiji hivyo kwa ajili ya kujitambulisha kwakuwa mkuu huyo wa wilaya ni mgeni baada ya kuhamishiwa hapo kutoka wilaya ya Kilombero

Herman Vedasto mkazi wa kijiji cha Mulungu na  Lazaro Jacob mkazi wa Bunyambo kata ya Samvula walisema kuwa kumekuwepo na tabia ya baadhi ya Askali polisi ambao wamekuwa wakiingia kwenye vijiji hivyo, na kuwa kamata wananchi bila sababu na kuwatesa  Walimuomba mkuu huyo wa wilaya kuhakikisha anazungumza na jeshi hilo, na kuhakikisha wanadhibitiwa na kuacha tabia ya kuwasumbua wananchi hali 

inayoondoa dhana ya utawara bora

Wamesema kuwa waonawaza bora wahamishwe katika kijiji hicho, waletwe watu wengine labda wao hawastaili kuishi katika eneo hilo cha Mulungu japo wanajitambua kuwa Raia halisi wa nchii hii kwa kuwa wanaishi kama wakimbizi bila amani kwenye nchi ,  alisema Herman Vedastor
Marko Joshua ambaye ni Kamanda wa polisi wilayani humo alipotakiwa kujibu tuhuma zinazoelekezwa kwa Askali wake alieleza   kuwa kila mtu anapaswa kutimiza sheria bila shuruti hakuana polisi ambaye yuko pale kwa ajili ya kusumbua wananchi na nivema wanapoona hali hiyo waeze kutoa taarifa katika ngazi zinazohusika kwa hatua zaidi

Nae mkuu wa wilaya hiyo Hassani Masala ameeleza kuwa, polisi ni chombo kilichopewa dhamana ya kuwalinda laia na mali zao lakini inapotokea Askali anavunja taratibu za kazi, yeye kama mkuu wa wilaya hatavumilia kuona  watu wanafanyiwa vitendo visivyostaili na kuwataka wananchi hao kutoa taarifa wanapokuwa wamefaniwa matendo mabaya na askali polisi yeyote ili atakapobainika hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi yake

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao