Makao ya kiongozi wa upinzani yazungukwa

Kiongozi wa upinzani nchini Sudan Kusini Lam Akol anasema kuwa nyumba yake imezingirwa na vikosi vya usalama na sasa yuko chini ya kuzuizi cha nyumbani.
Bwana Akol ambaye ni kiongozi wa Sudan People's Liberation Movement - Democratic Change, aliiambia BBC kuwa alikuwa amewasiliana na serikali ya Salva Kiir kuuliza ni kwa nini hatua hizo zimechukuliwa , lakini licha ya hilo bado hajapata jibu.
Lam Akol
Siku za hivi majuzi bwana Akol amekuwa akiilaumu vikali serikali ya Sudan Kusini kutokana na mipango ya kutaka kutumia karibu dola milioni mia mbili kwenye sherehe za kuadhimisha miaka minne ya uhuru wakati ambapo hali ya uchumi ni mbaya.
Jeshi la Sudan Kusini

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Matumizi ya simu kwa wanafunzi chanzo mmomonyoko wa maadili’

HATARI: Wengi wanunua sabuni za dawa bila maelekezo ya wataalamu

Wazazi timizeni wajibu wenu katika Malezi ili Watoto wenu wafikie Ndoto zao